Zaidi ya watu Bilioni Moja duniani wanaishi na ulemavu, na Umoja wa Mataifa unasema kuwa kila uchwao vita na mizozo vinaongeza hatari ya idadi ya walemavu kuongezeka.  Hivyo basi, bila jamii jumuishi, maendeleo endelevu yatakuwa ni ndoto na hata ndoto za walemavu kuweza kuwa na maisha bora yenye hadhi haitaweza kufikiwa.
Katika kuhakikisha jamii hiyo inajumuishwa kando mwa mjadala mkuu wa Baraza kuu mjini New York, kulifanyika mjadala wenye maudhui ya kuwa ulemavu si kushindwa kufanya jambo na miongoni mwa washiriki ni Henry Wanyoike, mwanariadha mashuhuri mwenye ulemavu wa macho kutoka Kenya, akiwa na msaidizi wake Joseph Kibunja. Assumpta Massoi alipata fursa ya kuzungumza nao na kwanza Wanyoike alielezea lengo la uwepo wao.

Kusikiliza mahojiano haya bofya  http://www.Radio.un.org/sw 



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...