Wachezaji wa timu ya Netiboli ya Utumishi na TASWA QEENS wakigombea mpira wakati wa mechi ya kirafiki iliyofanyika jana katika viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam. 
Utumishi iliibuka mshindi kwa mabao 43-19.
 Mchezaji wa timu ya Netobili ya Utumishi Anna Msolwa (kushoto) akitoa pasi wakati wa mechi ya kirafiki kati ya Utumishi na TASWA QEENS katika viwanja vya Leaders Club jijini Dar es Salaam.Utumishi iliibuka mshindi kwa mabao 43-19.
 Mojawapo ya magoli ambapo Utumishi iliibuka mshindi kwa mabao 43-19 dhidi ya TASWA QEENS.
Naibu Katibu Mkuu,Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma Bw.HAB Mkwizu (katikati) akiwapongeza wachezaji wa TASWA QEENS baada ya mechi ya kirafiki iliyofanyika jana viwanja vya Leaders Club kati yake na  Utumishi.
----------------------------
Timu ya Netiboli ya Utumishi imeendelea kujiweka sawa katika maandalizi ya mashindano ya SHIMIWI baada ya kuichapa TASWA Queens mabao 43 kwa 19 katika mechi ya kirafiki iliyokuwa na ushindani mkali  iliyofanyika katika viwanja vya Leaders Club jijini Dar es salaam jana jioni.
 Mechi hiyo iliyokuwa na ushindani wa aina yake, ilianza kwa kasi huku wachezaji wa pande zote mbili wakioneshana umahiri wao .
Iliwachukua takribani dakika 8 timu ya Utumishi kuumiliki mchezo katika kipindi cha kwanza na kubwagiza TASWA Queens mabao 22 kwa 10.
Kipindi cha pili kilianza kwa kasi ya kushambuliana kwa zamu huku kila timu ikitaka kujivunia idadi kubwa ya magoli mapema, ni Utumishi ndio walionufaika na mashambulizi hayo baada ya kufika kwenye goli la wapinzani mara 25 na kufanikiwa kupata mabao 21 bila ajizi.
Kwa upande wa TASWA Queens walifanya mashambulizi ya kutosha lakini ukosefu wa umakini wa GA na GS wao uliwagharimu, hivyo hadi mchezo unamalizika Utumishi waliibuka na ushindi  mnono wa magoli 43-19.
Wafungaji wa timu ya Utumishi walikuwa ni Fatma Ahmed aliyefunga mabao 25 na Anna Msulwa aliyefunga mabao 18.
Kwa upande wa timu ya TASWA wafungaji walikuwa ni Zainabu Ramadhani ambaye alifunga mabao 15 na Elizabeth Mbasa ambaye alifunga mabao 4.
Akizungumza baada ya kumalizika kwa mchezo huo Naibu Katibu Mkuu,Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma B.HAB Mkwizu alisema timu ya Utumishi inatakiwa iongeze muda wa kufanya mazoezi zaidi ili iweze kufanya vizuri katika mashindano ya SHIMIWI yajayo  yanayotarajiwa kufanyika Septemba hii mjini Dodoma.
“Muongeze muda wa mazoezi ili mjiongezee stamina na pumzi ya kutosha kwa ajili ya mechi zijazo”alisema Bw.Mkwizu.
Aidha, Bw.Mkwizu alimtaka kocha wa timu hiyo Bw.Mathew Kambona kufanya marekebisho ya makosa ya  kiufundi yaliyojitokeza uwanjani wakati wa mechi hiyo ili kuijenga timu kiufundi.
Naye kocha mchezaji wa TASWA Queens Bi. Zainabu Ramadhani mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo aliipongeza timu ya Utumishi kwa kuwa na wachezaji  wazuri na kuitaka timu hiyo kujiimarisha zaidi katika upande wa ulinzi.

Timu ya Utumishi iko kwenye maandalizi ya mwisho kwa ajili ya kushiriki mashindano ya SHIMIWI yanayohusisha watumishi wa Idara za Serikali na Wizara yatakayofanyika viwanja vya UDOM mjini Dodoma hivi karibuni.



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...