Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Mhe. Bernard K. Membe (Mb.) akizungumza na Mhe. Tuvako Manongi, Balozi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa mjini New York alipofika Ofisini kwake kabla ya kukutana na Wafanyakazi wa Ubalozi huo.

Mhe. Membe akizungumza na Wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania Mjini New York (hawapo pichani) alipokuwa mjini humo kuhudhuria Kikao cha 68 cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa.
Mhe. Balozi Manongi akimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) alipozungumza nao. Kulia kwa Balozi ni Bi. Rose Mkapa, Kaimu Mkuu wa Utawala Ubalozi akifuatiwa na Bw. Justine Kisoka na Bi. Ellen Maduhu, Maafisa katika Ubalozi huo.
Mkurugenzi wa Idara ya Ushirikiano wa Kimataifa katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Balozi Celestine Mushy  wa kwanza kushoto akimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani) alipozungumza na Wafanyakazi wa Ubalozi wa Tanzania, New York. Kushoto kwa Balozi Mushy ni Dkt. Justin Seruhere akifuatiwa na Bi. Maura Mwingira na Bw. Noel Kaganda Maafisa katika Ubalozi huo.
Bw. Yusuph Tugutu (kulia), Afisa katika Ubalozi akimsikiliza Mhe. Membe (hayupo pichani)akifuatiwa na Bw. Togolani Mavura, Msaidizi wa Mhe. Waziri, Bw. Grayson Ishengoma, Afisa Mambo ya Nje kutoka Wizarani na Bi. Tully Mwaipopo, Afisa katika Ubalozi. Picha na Rosemary Malale

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...