Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akiongoza kikao kati ya balozi wa Tanzania nchini Congo DRC Balozi Anthony Cheche aliyefika ofisini kwake kwa lengo la kujitambulisha na kujadili mambo mbalimbali ya kimahusiano kati ya nchi hizo mbili. Mkuu huyo wa Mkoa alimuomba balozi Cheche kunadi fursa za uwekezaji zinazopatikana Mkoani Rukwa pamoja na kuunganisha nguvu ya nchi hizi mbili katika kuwekeza kwenye usafiri wa majini katika Ziwa Tanganyika. Akizungumzia kuhusu wahamiaji haramu amesema ni bora kujenga ushirikiano mzuri wa kibiashara kwa nchi zote mbili ambapo taratibu maalum zitafuatwa kwa wananchi na wafanyabiashara kuingia na kutoka. 

Balozi Anthony Cheche anayoiwakilisha Tanzania nchini DRC akizungumza Ofisini kwa Mkuu wa Mkoa wa Rukwa leo alipoonana na uongozi wa Mkoa kwa lengo la kujitambulisha na kujadili mambo kadhaa ya mahusiano kati ya Tanzania na Congo DRC. Ameiomba Serikali ya Tanzania kuangalia upya vizuizi vya njiani kwa wafanyabiashara wa nje ikiwemo DRC hususani uwepo wa mizani nyingi barabarani na badala yake ziwepo chache na ziwe mbali kidogo na barabara kuepusha usumbufu kwa wasafiri wengine na wafanyabiashara.
Baadhi ya wakuu wa idara katika Sekretarieti ya Mkoa wa Rukwa wakiteta jambo katika kikao hicho, Kulia ni Katibu Tawala Msaidizi Utawala na Rasilimali Watu Ndugu Samson Mashalla, Kaimu Katibu Tawala Msaidizi Idara ya Mipango Ndugu David Kilonzo na Kaimu Katibu Tawala Idar a ya Uchumi na Uwezeshaji Ndugu Respitch Maengo. 
Picha ya pamoja.(Picha na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa @Rukwareview.blogspot.com)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...