MBU ni tatizo kubwa kwa afya zetu na familia zetu kwa ujumla.Tokomeza maleria kwa kutumia dawa ya asili iliyotengenezwa kwa mitishamba Dawa hii ukishaiweka kwenye umeme inatoa harufu nzuri isiyokuwa na kero, ambapo husababisha mbu kuikimbia harufu hiyo. 
Unaweza kuacha mlango wazi na mbu hukimbia kwenda nje, na walio nje hawewezi kuingia ndani kutokana na perfume inayotoka kwenye dawa hii. Kumbuka kuwa mbu huingia ndani kwa wingi mida ya jioni giza linapoanza na asubuhi kunapoanza kupambazuka, muda huo kama utakuwa umewasha dawa, hata ukifungua milango mbu hawataingia ndani. Haina madhara kwa afya ya mwanadamu kwa kuwa imetengenewa kwa miti shamba na products nyingine za asili.
Machine pamoja na dawa Tsh 25,000/=. Dawa (liquid) peke yake Tsh 10,000

Sabuni bei yake ni 5000/=.sabuni hii haina madhara hata kwa mtoto mchanga imetengenezwa kwa miti shamba. Hii ni Sabuni nzuri sana kwa ajili ya kufukuza mbu, ukiitumia kwa kuoga inaacha harufu mwilini ambayo mbu huikimbia harufu hiyo. Sabuni hii pia ni nzuri kwa ngozi, pimples na mabaka/madoa kwenye ngozi huondoka. Haina madhara kwa afya ya mwanadamu kwa kuwa imetengenewa kwa miti shamba na products nyingine za asili. Mtoto mdogo anaweza kuitumia sabuni hii. Familia yangu tunatumia sabuni hii.

Kwa anayetaka kuwa supplier au kununua 
kwa bei ya jumla naomba tuwasiliane pia.
 — at Mwenge Near TRA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. Tuambie kuhusu kuthibitishwa na TBS

    ReplyDelete
  2. Watu wengu wana aleji ya pafume. Je hii haitawadhuru?

    Je ina viwango vilivyopimwa?

    ReplyDelete
  3. Mti upi? Na pia TFDA wameithibitisha mana isije ikawa kama ya mafuta ya ubuyu, yale yale! watu watumie mwisho wa siku oh haifai kwa matumizi ya binadamu. Mana huo moshi wake ndio mpango mzima katika kuvuta, je mwilini hakuna tatizo, mdau juu
    alivyosema allergies nk?

    ReplyDelete
  4. Je, imethibitishwa na TBS? Maana kutengeneza na miti shamba si hoja. Kwa kuwa dawa nyingi zinatokana na miti shamba, isipokuwa zinawekwa ktk maumbo fulani fulani kwa kutumia mashine.

    Mimi utaweza kunishawishi utakapoonesha alama ya TBS

    ReplyDelete
  5. Nyinyi mmesoma Maelezo!! Mshaambiwa haina MADHARAAA!!!

    ReplyDelete
  6. Sio mtu atuambie haina madhara maana kila mfanya biashara atasema hivyo, tunataka tuambiwe na trusted source kama TBS, TFDA n.k. Apeleke hiyo perfume na sabuni vikafanyiwe utafiti.......

    ReplyDelete
  7. ni kweli kabisa kupata uthibitisho kutoka taasisi za Serikali sio kwa mfanyabiashara kwa maneno ya kibiashara.

    ReplyDelete
  8. Hebu wa-scan vyeti vya TFDA na TBS tupate uhakika.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...