Kamishna Msaidizi wa Madini, Hamis Komba akitoa maelezo kwa mkuu wa wilaya ya Namtumbo Bw. Abdula Lutavi juu ya lengo la Wizara ya Nishati na Madini la kutoa elimu ya urani katika wilaya ya Namtumbo mkoani Ruvuma.
Kamishna Msaidizi wa Madini, Hamis Komba ( wa kwanza kulia) akiwa na viongozi mbalimbali waliohudhuria warsha kuhusu elimu ya urani kwa wananchi wa wilaya ya Namtumbo. Kushoto kwa Kamishna ni Mkuu wa Wilaya ya Namtumbo, Abdula Lutavi.
Wananchi wa wilaya ya Namtumbo wakisikiliza moja ya mada iliyokuwa ikitolewa katika warsha hiyo
Wananchi wakipita kuangalia sampuli ya madini ya Urani. Sampuli hiyo ililetwa kwenye warsha hiyo ili kuwaonesha kwa vitendo wananchi kuwa mionzi ya madini hayo yakiwa ghafi, haina madhara kwa afya za wananchi.
Wananchi wakipita kuangalia sampuli ya madini ya Urani. Sampuli hiyo ililetwa kwenye warsha hiyo ili kuwaonesha kwa vitendo wananchi kuwa mionzi ya madini hayo yakiwa ghafi, haina madhara kwa afya za wananchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...