Na Abdulaziz Video, Lindi
Mtu mmoja aliejulikana kwa jina la Burhan Islam ambaye ni fundi wa magari, amenusurika kifo baada ya gari alilokuwa akisafiria aina ya Fuso kugonga lori lingine nae kubanwa na bodi na kuokolewa baada ya jitihada zilizofanywa na baadhi ya Abiria waliokuwa wakisafiri katika barabara kuu ya Dar es salamu kwenda Mtwara na Lindi.
Gari hilo lenye namba za usajiri T 56ANQ lililokuwa likiendeshwa na Kunja Mshamu limepata ajali hiyo leo katika kijiji cha Mkwajuni wilayani Lindi baada ya kutaka kulipita gari lenye namba za usajili T 402 AJG Scania lililokuwa likiendeshwa na Amos Chadenyile.
Majeruhi huyo baada ya kuokolewa katika ajali hiyo alikimbizwa katika kituo cha afya Kitomanga kwa huduma ya kwanza kabla ya kupelekwa katika hospital ya Mkoa wa Lindi kwa Uchunguzi zaidi. Katika ajali hiyo iliyousisha malori hayo hakuna mtu mwingine aliyejeruhiwa huku gari hiyo ya Fuso likiwa limeharibika sana
Wasamaria wakifanya juhudi za kumnasua Burhan Islam


Majeruhi Burhan Islam baada ya kuchomolewa sehemu aliyokuwa amenasa na kabla ya kukimbizwa kituo cha afya kwa huduma ya kwanza

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Pole sana Burhan - Mungu ameyanusuru maisha yako!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...