MAREHEMU MZEE ASHERI A.M. MWASANDUBE

 Siku, miezi na sasa mwaka mmoja umetimiza tangu Mwenyezi Mungu akuite nyumbani.   Alhamisi ya tarehe 11 Oktoba, 2012 ilikuwa ya majonzi makuu katika familia yetu, Bwana alipotazama shambani mwake akaona nafasi, kisha akatazama duniani na kukuona baba yetu mpendwa ukiwa taabani pale Muhimbili Hospitali, ndipo alipokukumbatia na kukuambia ASHERI Mwanangu inatosha njoo nyumbani.

Hakika bustani ya Bwana yapendekeza imesheheni watu wake walio bora, wampendezaye.  Nasi tunazidi kumshukuru Mungu kwa zawadi ya maisha haya, tangu tulivyokuwa nawe kimwili hadi sasa ambapo unaendelea kudumu nasi kiroho.

unakumbukwa sana na familia yako Mama ELESIA KATAPA, Watoto wako Hilda, Sarome, Stephen, Sekela, Abrahamu, wajukuu zako, dada zako, wadogo zako, ndugu, majirani kila mmoja kwa namna ya pekee.

Kwetu Baba yetu mpendwa unaendelea kudumu katika kila pumzi ya uhai wetu, tunaendelea kusimama katika misingi uliyoiweka tena bila kutetereka, tukitumaini kuwa siku moja tutaungana nawe katika kiti cha enzi cha Bwana  wetu Yesu Kristo.  "AMEN"

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...