Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (kushoto) akipokea zawadi kutoka kwa Meya wa mji wa Hammerfest ulioko Norway, Alf Jakobsen. Waziri aliongoza Ujumbe kutoka Tanzania katika ziara ya mafunzo nchini Norway hivi karibuni, kuhusu namna ambavyo sekta ya gesi inaweza kutumika kukuza uchumi wa nchi.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo akisalimiana na Meya wa mji wa Sandnessjoen nchini Norway, Bard Anders alipofika ofisini kwake kwa mazungumzo. Waziri na Ujumbe kutoka Tanzania walitembelea nchini humo hivi karibuni kwa ziara ya mafunzo kuhusiana na gesi asilia.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (mwenye koti refu) akijadiliana jambo na Meya wa mji wa Sandnessjoen, Bard Anders (kulia kwa Waziri) na Balozi wa Norway nchini Tanzania, Ingunn Klepsvik (wa kwanza kushoto.) Waziri Muhongo na Ujumbe wake walikuwa katika ziara ya mafunzo ya gesi asilia nchini Norway hivi karibuni.
Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo (mstari wa mbele-katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Ujumbe ulioongozana naye katika ziara ya mafunzo kuhusu gesi asilia nchini Norway, pamoja na wenyeji wao mjini Sandnessjoen.
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
BOFYA HAPA KWA PICHA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...