Ankal salam. Wasafiri na wasafirishaji katika barabara zetu hupata usumbufu mkubwa sana wanapofika kwenye upimaji wa magari yao katika weigh-bridge (mizani za kupima Magari). Wenzetu kwenye nchi zilizoendelea wamefikia kuwa na technology ambayo mizani hizo hazina operator (yaani ni unattended). 
Yaani dereva akifika katika mizani na truck yake, anaingiza kadi yake kwenye mashine iliyopo hapo (kama tufanyavyo pale airport), halafu gari hupimwa automatically na kumbukumbu zote kuwafikia wahusika kwa mtandao immediately. Nadhani Tanzania inahitaji mfumo wa kisasa kama huo, ili kuondoa usumbufu uliopo huko kibamba, mikese, Msata, etc. 
 Eid njema Ankal. 
 Mdau Sent from my iPad

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. Kweli ni wazo zuri sana mdau,tena la kimaendeleo,ila kwa bongo huo usumbufu unauona upo hapo kwa faida ya watu,hawatapenda uondoke maana ni mradi.

    ReplyDelete
  2. Tanzania kufikia hapo itakuwa ni hatua kubwa sana kimaendeleo.Hivi ni vitu vidogo sana bado vinatushinda.Mbali ya usumbufu wa mizani, foleni za magari kila mahali, barabara finyu na mbovu, njia za mkato zipo lakini ni mbovu na hazipitiki.

    ReplyDelete
  3. Mizani ijiendeeshayo yenyewe ya kupimia magari.

    ReplyDelete
  4. Mizani ijiendeeshayo yenyewe ya kupimia magari.

    ReplyDelete
  5. Jameni mkifunga mitambo hiyo ya kisasa watu 'watakula' wapi?

    ReplyDelete
  6. Hii pia itaondosha wizi unaofanywa na watendaji walioko kwenye mizani

    ReplyDelete
  7. Kwenye mizani wanatakiwa labda askari tu lakini mizani ikiungwa na mtandao wa internet hadi kwenye mamlaka wizi wote utaisha, sema tu wabongo tunapenda mno longo longo

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...