Muuguzi wa Hospitali ya Tanwat, Asnath Mdakule akitoa huduma ya upimaji wa afya ya magonjwa ya shinikizo la damu ‘BP’ na uwiano kati ya urefu na uzito kwa mmoja wa wananchi waliotembelea banda la Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), wakati maonesho ya uzinduzi wa mkoa mpya wa Njombe, ikiwa ni moja ya huduma zinazotolewa na shirika hilo katika mafao ya Matibabu. (Picha na Shaban Lupimo)
 Muajiri Mkubwa wa NSSF Njombe ambae ni  Mhandisi wa kampuni ya Tanwat Njombe Umesh Radd akisaini kitabu cha wageni kabla ya kupokea maelezo kuhusiana na uanachama wa hiari na sekta binafsi kutoka  kwa Meneja wa Shirika la Hifadhi ya Jamii NSSF mkoa wa Njombe, Godwin Mwakalukwa baada ya kutembelea banda la shirika hilo kwenye maonesho ya uzinduzi wa mkoa katika uwanja wa. 
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Kapteni Mstaafu Aseri Msangi (kushoto) akipokea maelezo kuhusiana na uanachama wa hiari na sekta binafsi kutoka  kwa Meneja wa Shirika la Hifadhi ya Jamii NSSF mkoa wa Njombe,Godwin Mwakalukwa (katika) baada ya kutembelea banda la shirika hilo kwenye maonesho ya uzinduzi wa mkoa katika uwanja wa SabaSaba kulia ni Ofisa Uhusiano wa shirika hilo Maife Kapinga. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...