Na Ripota wa Globu ya Jamii, Nairobi
Mheshimiwa Prof. Mark J. Mwandosya(MB), Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Kazi Maalum yuko katika ziara ya kikazi hapa Nairobi kuanzia tarehe 7 Oktoba, 2013 akiongoza ujumbe wa watu sita kutoka Taasisi mbalimbali za Udhibiti. 
Akiwa hapa Nairobi, Mheshimiwa Waziri Mwandosya atatembelea Wizara na Taasisi zinazujishughulisha na Udhibiti wa huduma katika sekta za umeme, maji, ‘gesi, mwawasiliano, usafiri wa anga, majini na nchi kavu pamoja na Taasisi ya Uwekezaji ya Kenya. 
 Katika siku yake ya kwanza ya ziara yake tarehe 7 Oktoba, 2013, Mheshimiwa Mwandosya na Ujumbe wake alikutana na uongozi wa Maalaka ya Uwekezaji wa Kenya (Kenya Investment Authority), ukiongozwa na Dkt. Moses Ikiara, Managing director. 
 Pia alikutana na Mheshimiwa Dkt. Fred Matiangi, Waziri wa Mawasiliano wa Kenya. Mheshimiwa Waziri Mwandosya leo atakutana na uongozi wa Energy Regulatory Commission, Communication Commission of Kenya (CCK), pamoja na National Communication Secretariat
Profesa  Mwandosya akipata ufafanuzi kutoka kwa Dkt. Moses Ikiara, MD wa Kenya Investiment Authority  kuhusu utendaji wa Mamlaka ya Uwekezaji, changamoto zilizopo na mwelekeo wa baadaye wa mamlaka hiyo
Profesa Mwandosya akimkabidhi kitabu shake Dkt. Moses Ikiara, MD wa Kenya Investiment Authority  
Profesa  Mwandosya katika Picha ya pamoja na timu ya Uongozi ya malaka ya Uwekezaji Kenya pamoja na ujumbe wake alioongozana nao.
Profesa andosya akiwa na Mh. Dkt. Fred Matiang'i, Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia wa Kenya alipomtembelea ofisini kwake leo. Profesa  Mwandosya anakutana na Taasisi zote za Udhibiti ambazo ziko chini ya Wizara hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...