Sr Consolata Shayo 30 Mei 1935 – 15 Oktoba 2013
Mama mlezi, Mkuu wa Shule ya Wasichana Kibosho Sekondari kwa muda mrefu sana kuanzia miaka ya 1960 mpaka 1990. Mama, umetulea, umetutunza, umetujengea uwezo, umetuonyesha njia ya maisha bora. Sasa siku nyingine imefika, tuko hapa peke yetu, tumebaki na masikitiko, haupo tena na sisi. Ulikuwa mara nyingi ukisema kwaheri, na wengine tulikuuliza kwa nini? Kweli sasa umeondoka na kutuacha na mstuko. Machozi yanatutoka katika hali ya kibinadamu lakini tunashukuru, mapenzi ya Mungu yatimizwe.
Hata hivyo tunafarijika tukifikiri kuwa, kwa kazi kubwa uliyofanya duniani, ikatoa wanawake jasiri kama sisi, sasa upo katika pumziko la milele na Mungu na Malaika wa Mbinguni. Kimwili umetutoka, lakini kiroho bado upo hai katika kumbukumbu zetu.
Katika hali hii, hatujabaki peke yetu, bado upo mama. Ingawa uko mbali na macho yetu, kumbukumbu yako bado inaishi. Tulibarikiwa sana na tunamshukuru Mungu kwani alitupa bahati ya kulelewa na wewe mama Consolata na kutokana na malezi yako tumejifunza jinsi ya kuwa mfano bora wa mama. Watoto wetu wanafaidi malezi yako, na tunaamini watayapeleka kwa wana wao hivyo kwa jinsi hiyo kumbukumbu yako itaendelea kuishi na kutoa Baraka vizazi hata vizazi. Mama,kwaheri. Tunakuombea Mola akupe mapumziko mema. Amen!
Mother tuko hapa tulipo kwa kupitia mikono yako. Mother ulitupenda, ulitulea, ulitusindikiza katika njia ya mafanikio. RIP mother Consolata
ReplyDeleteDr. Ave Maria Semakafu
Mama yetu mpendwa hatutakusahau katika maisha yetu mafanikio yetu ni wewe Mama yetu mpendwa ulitufundisha mengi sana ambayo hayaelezeki. Tuko pamoja na familia katika kipindi hiki cha huzuni.
ReplyDeleteJamani, Mother Conso,hatuna jinsi ya kusema ni namna gani tumeumia lakini ni kukuombea upumzike kwa amani. Mama ulitulea kama watoto wako wa kutuzaa pale Kibosho,ulitupenda na ukaweka upendo kati yatu kama familia moja. Kweli tunajivunia sana upendo,upole,ujasili,usafi na kujiamini uliotujengea mama unatusaidia sana katika maisha yetu,katika familia zetu na katika nyumba zetu, Ulikuwa mama mwema kwetu kwa wote tuliopita katika mikono yako.Tunakuombea mama upumzike kwa amani.R.I.P Mother Conso.
ReplyDeleteRosemary Makene
Kwa kweli tumesikitika sana,hatuna hata namna ya kuelezea masikitiko yetu.Tunamwomba mwenyezi Mungu akupumzishe kwa amani katika makao ya Milele.''Raha ya Milele Umpe e Bwana na Mwanga wa Milele Umwangazie ,Apumzike kwa Amani -Amina''
ReplyDeleteMartina Massawe
Jamani mama!!roho ziatuuma lakini hatuna jinsi,upumsike kwa amani mama,mama wetu wa upendo conso...tulikupenda mama lakini mwenyenzi mungu alikupenda zaidi...jina la bwana libarikiwe..pumzika kwa amani mama..
ReplyDeleteLillian Urasa sweden
Jamani Mother Conso wetu, tulikupenda ila Mungu kakupenda zaidi. Ulale kwa amani mama yetu mpendwa. Upendo wako kwetu hauna maelezo,malezi yako mema yametufanya nasi kuwa mama wema na wajasiri. Ulitupa misingi mizuri katika maisha yetu ambayo tutajivunia daima. Ulitulea kama watoto wako binafsi. Rest in peace Mother Consolata.
ReplyDeleteSusan Mrango.
Nilifikiiri sr fidesta wa kifungilo.poleni watoto wakibosho maana I can't imagine to loose our mother too sr fidesta
ReplyDeleteMother Consolata tutakumiss na kukumbuka daima, ulikuwa kioo cha maisha na ulitupa elimu bila ubaguzi tuitumie na iwe ufunguo wa Maisha. Aliyeyapokea maneno yako kwenye assembly point ameweza kuishi na kujiheshimu kufanikisha adhima ya maisha yake.. Hatutakusahau kamwe na usemi wako "mmenisikia vijana"... assembly dismiss. RIP Maza Conso. Laura Doris Shao
ReplyDeleteWahenga wanasema nani kama mama hakuna basi Mother ulkuwa ni mama wa kipekee. Tulipokuwa katika mikono yako oooh tulideka tulipata maadili mazuri na hatimaye tulijengeka na kujua ni namna gani tunaishi katika jamii kama kioo cha maendeleo
ReplyDeleteMwenyezi akupe raha ya milele
Mama yetu mpendwa Consolata Shayo, ni huzuni isiyoelezeka kututoka tukiwa bado tunakupenda sana. Ulikuwa Kiongozi Jasiri na Mama Shujaa. Ulitupa misingi Imara tunayojivunia kama wamama shujaa wa Africa, asante kwa urithi wa malezi bora tunayoendelea kuwarithisha wanajamii wote.Tutakuenzi daima kwa vitendo kwa kuwa mifano bora na yakuigwa popote pale tutakapokuwa. Mungu akupe pumziko la amani na mwanga wa milele akuangazie mpendwa wetu Mother Consolata. Poleni sana wanafamilia na wana wa Kibosho girls' Sec School 1960s - todate.
ReplyDeleteCathy Mworia.
Kimwili umetuacha lakini maadili yako hayatatuacha kamwe.
ReplyDeleteMama yetu mpendwa Consolata Shayo, ni huzuni isiyoelezeka kututoka tukiwa bado tunakupenda sana. Ulikuwa Kiongozi Jasiri na Mama Shujaa. Ulitupa misingi Imara tunayojivunia kama wamama shujaa wa Africa, asante kwa urithi wa malezi bora tunayoendelea kuwarithisha wanajamii wote.Tutakuenzi daima kwa vitendo kwa kuwa mifano bora na yakuigwa popote pale tutakapokuwa. Mungu akupe pumziko la amani na mwanga wa milele akuangazie mpendwa wetu Mother Consolata. Poleni sana wanafamilia na wana wa Kibosho girls' Sec School 1960s - todate.
ReplyDeleteCathy Mworia.
Tunakushukuru Mama kwa kutujenga, japo wakati ule tulikushangaa ulivyokuwa mkali lakini sasa tunatambua ulikuwa upendo wetu kwetu. Tunashukuru pia kutupa nafasi ya kukuhudumia na hata kukuona ulipoturuhusu kukuleta Dar kwa matibabu. Mama tulikupenda ila Mungu ameona unahitaji pumziko. Asante kwa yote. Pumzika kwa amani Mama, wanao umetupa yote tunaweza kusisimama.
ReplyDeleteXkibosho
Bibi Yangu Mpendwa ulinilea katika misingi yote ya kidini na malezi mazuri sina cha kukulipa na sitaweza kukulipa zaidi ya kukuombea tu Bibi yangu Mpendwa ukapumzike salama Bibi.
ReplyDeleteTunakukumbuka sana sisi wajukuu zako. Ukapumzike kwa Amani.
Mungu uweke moyo wa mpenzi mpendwa mama mahali pema. Namshukuru mungu kuwa miongoni mwa uangalizi wako. Ulijitolea asilimia 100 kutuangalia na kila ulolifanya uliku ukifanya kwa faida ya watoto wako. Kumbukumbu nyingi ninazo hasa ulipokuwa ukirudi safari , tukiona gali tunakimbilia tukipiga makelele" mama mama " siku inayofwata tunakua na assembly unatueleza kuhusu safali yako na kusema umefanikiwa nini kuhusu maendeleo ya shule . Umeacha Kumbukumbu ambayo itaendelea milele na milele. Mapumziko mema, Amen
ReplyDeleteNashukuru kwa kwa huduma hii.
ReplyDeleteAsante
ReplyDeleteAsante kwa huduma hii
ReplyDelete