Bango maalum lililoandaliwa na Mtanzania kwa Watanzania katika hafla ya kumbukumbu ya Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere maafuru kama Mwalimu Nyerere Day iliyofanyika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York Jumatatu Oktoba 14, 2013
Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi akiashiria uzinduzi wa uzinduzi wa
kitabu kilichopewa jina "Julius Nyerere African's Titan on a Global State:
Perspective from Arusha to Obama" kilichoandikwa kwa pamoja kati ya
Mwanazuoni Maarufu Professa Ali Mazrui na Professa Lindah
Mhando.
Professa Ali Mazrui akionyesha kitabu kuhusu Mwalimu Nyerere
ambacho yeye na Profesa Lindah Mhando wamekiandika
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Jan Elliasson
ambaye alikuwa mgeni rasmi akizungumza wakati wa hafla hiyo ya Mwalimu Nyerere
Day pembeni yake ni Mwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,
Balozi Tuvako Manongi. Chini ni sehemu ya umati uliohudhuria
Uwakilishi wa
Kudumu wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa,
kwa mara ya kwanza umeadhimisha kwa namna ya pekee kumbukumbu ya Baba wa
Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere maafuru kama Mwalimu
Nyerere Day.
Hafla hiyo imefanyika siku ya Jumatatu
hapa Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa na mgeni Rasmi alikuwa Naibu
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw. Jan Eliasson ambaye alimwakilisha
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa. Hafla hiyo pia iliendana na uzinduzi
wa kitabu kilichopewa jina "Julius Nyerere African's Titan on a Global State:
Perspective from Arusha to Obama" kilichoandikwa kwa pamoja kati ya
Mwanazuoni Maarufu Professa Ali Mazrui na Professa Lindah
Mhando.
Wageni mbalimbali wakiwamo mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao katika
Umoja wa Mataifa walipata fursa ya kutoa salamu zao zilizosheheni masuala
makuu ambayo Baba wa Taifa enzi za uhai wake aliyasema kwa
nguvu zake zote, masuala ambayo kwa mujibu wa wazungumzaji
hao mengi kati yake yanaendelea kutekelezwa au kuzungumziwa
hata sasa katika duru za kimataifa, ni pamoja na uhuru
na utu wa mtu mweusi, maendeleo shirikishi yakiwamo malengo ya
maendeleo ya millenia , kupiga vita umaskini, magonjwa na matumzi
ya silaha kali kama vile silaha za nyuklia, alikuwa
mstari wa mbele katika kuhakikisha nchini nyingi hasa
zile za kusini mwa afrika zinapata uhuru wake na vilevile alikuwa
kiongozi aliyeona mbali na aliyeweza kuwaunganisha siyo tu watanzania
bali hata waaafrika wengine.
Kwa
taswira zaidi ya tukio hilo pamoja na Salamu za Naibu Katibu Mkuu
wa Umoja wa Mataifa na wazungumzaji wengine:
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...