Mtoa mada na Mtafiti wa Ugonjwa wa Kifua Kikuu(TB)Dr Said Egwaga akizungumza na waandishi wa habari leo katika Hoteli ya Ngurdoto mkoani Arusha juu ya utafiti walioufanya mwaka 2011 katika wilaya 62 nchini ulibaini  kati ya watu Laki moja kuna wagonjwa wa Kifua Kikuu 295 na waliothirika zaidi ni wanaume ukilinganisha na wanawake na idadi kubwa iko maeneo ya  Vijijini  ukilinganisha na  mijini tofauti na walivyotarajia.
Mratibu wa Magonjwa yasiyopewa Kipaumbele nchini.Dr Upendo Mwingira akifafanua jambo kwa waandishi wa habari katika mkutano wa Kimataifa  cha taasisi za afya za jamii unaofanyika mkoani Arusha.
Wataalamu wakifatilia mada zilizokua zikiwasilishwa na mabingwa wa tafiti za magonjwa ya binadamu leo
Wataalamu wakifuatilia mada zilizokua zikiwasilishwa na mabingwa wa tafiti za magonjwa ya binadamu leo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Tanzania oyeeee....tuzidi kupambana na haya magonjwa.

    ReplyDelete
  2. Ukiboresha nyumba vijijini na kuondoa umasikini utabadilisha takwimu hizi kirahisi sana.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...