Na Dixon Busagaga
wa Globu Jamii, Moshi
wa Globu Jamii, Moshi
WATUHUMIWA saba wa mauaji ya mfanyabiashara wa madini ya tanzanite,
Erasto Msuya (43) wakiwemo wafanyabiashara maarufu wa madini hayo,
Joseph Damas “Chusa” na Sharif Mohamed Athuman wote wakazi wa Jiji la
Arusha jana wamefikishwa mbele ya Mahakama ya Hakimu Mkazi ya Moshi.
Watuhumiwa hao wote kwa pamoja walifikishwa mahakamni hapo wakiwa
katika gari maalumu la kubeba watuhumiwa majira ya saa 5:30 asubuhi
wakiwa chini ya ulinzi mkali wa polisi wenye silaha, wakiwemo wa
kikosi maalumu cha kutuliza ghasia (FFU).
Wakiwa katika chumba cha mahakama kilichowezesha watu wachache kuingia
ndani, mwendesha mashitaka wa serikali, wakili Stella Majaliwa baada
ya kutaja makosa yanayowakabili washitakiwa aliomba kuahirishwa kwa
kesi hiyo kutokana na kutokamilika kwa upelelezi.
Wakili Stella aliieleza mahakama hiyo kuwa washitakiwa hao
walifikishwa mahakamani hapo kutokana na kesi ya mauaji ya kukusudia
kinyume na kanuni namba 16, kifungu cha 196 ya sheria za makosa ya
jinai.
Kutokana na ombi hilo, hakimu mkazi wa mahakama ya hakimu mkazi Simon
Kobelo aliridhia na kupanga tarehe nyingine.
Kesi hiyo sasa itatajwa tena Oktoba 15 mwaka huu wakati washitakiwa
wote wamerudishwa mahabusu.
Mara ya kwanza washtakiwa hao walifikishwa mahakamani hapo Agosti 21, mwaka huu.
Wahitakiwa wengine katika kesi hiyo ni Shaibu Mpungi, Musa Mangu,
Jalila Zuberi, Sadiki Jabiri na Joseph Mwakipasile.
Mfanyabiashara Erasto Msuya aliuawa Agosti 7, mwaka huu majira ya 6:30
mchana kwa kupigwa risasi 13 kifuani, kando ya barabara kuu ya Arusha
– Moshi katika eneo la Mjohoroni, Wilaya ya Hai, karibu na Uwanja wa
Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA)
Watuhumiwa wa mauaji ya
mfanyabishara wa madini ya Tanzanite jijini Arusha,Erasto Msuya
wakifikishwa katika mahakama ya Hakimu Mkazi ya Moshi, mkoani Kilimanjaro. Picha na Dixon Busagaga
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...