WAZIRI MKUU Mizengo Pinda ameahidi kutoa fedha za kununua mizinga kati ya 100 na 200 kwa ajili ya wanakijiji wa Biturana, wilayani Kibondo, mkoani Kigoma ambao wanajihusisha na uhifadhi wa misitu pamoja na ufugaji nyuki.
Ametoa ahadi hiyo jana mchana (Alhamisi, Oktoba 3, 2013) wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa kijiji hicho mara baada ya kukagua eneo la hifadhi ya Biturana pamoja na baadhi ya mizinga iliyomo kwenye hifadhi hiyo.
Alisema kwa vile mizinga hiyo inatengenezwa kwenye wilaya yao kwa thamani ya sh. 50,000 kwa kila mzinga, atawatafutia fedha za kutosha mizinga 100 -200 kulingana na mahitaji yao ambazo ni kati ya sh. milioni 5/- na sh. milioni 10/-.
Waziri Mkuu aliwashauri waanze taratibu kuachana na mizinga ya asili na badala yake watumie mizinga ya viunzi na baada ya muda wakishaizoea itabidi wahamie kwenye mizinga ya biashara.
wee mbona tumbo limeniuma nilivyosoma
ReplyDeletemizinga ya kisasa, nikadhani mizinga ya kivita. baada ya kusoma vizuri nikagundua kuwa ni mizinga ya nyuku.
phew!!
mdau
Ukerewe