WAZIRI MKUU Mizengo Pinda amemtaka Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma kuhakikisha kuwa anafuatilia suala la mkopo kwa ajili ya ujenzi wa soko la Kagunga hadi alikamilishe.
Ametoa agizo hilo jana jioni (Jumanne, Oktoba mosi, 2013) wakati akizungumza na mamia ya wakazi wa kata ya Kagunga mara baada ya kuweka jiwe la msingi la soko la kimataifa la Kagunga ambalo liko umbali wa kilometa 1.5 kutoka mpakani mwa Tanzania na Burundi kwenye mwambao wa Ziwa Tanganyika.
Waziri Mkuu alisema kukamilika kwa ujenzi wa soko hilo kutatoa fursa za kibiashara baina wakazi wa Kagunga na vijiji jirani pamoja na nchi ya Burundi ambayo milima yake inaonekana kutokea mahali soko lililojengwa. Mji wa karibu na Kagunga ni Nyanza Lac ulioko kwenye jimbo la Makamba, nchini Burundi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...