Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania London unawakaribisha Watanzania wote watakaoweza kupata fursa kuja kuzungumza na Waziri wa Sheria na Katiba, Mheshimiwa Mathias Chikawe na Wawakilishi kutoka Wizara ya Sheria na Katiba - Tanzania, hapa Ubalozini siku ya Ijumaa (tarehe 01 Novemba 2013) kuanzia saa Tisa alasiri (15:00).
Mheshimiwa Waziri anatarajiwa kuzungumzia masuala mbalimbali ya Sheria na mchakato wa mabadiliko ya Katiba ya Tanzania unaondelea hivi sasa.
Mhe. Waziri Chikawe anatarajiwa kujibu maswali mbalimbali kutoka kwa wananchi watakaohudhuria mkutano huo.


IMETOLEWA NA UBALOZI WA TANZANIA NCHINI UINGEREZA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. MIMI NAKWENDA KUPIGA MABOX LONDON UNDERGROUND NIKIMALIZA MAPEMA NITAKIJA.MDAU LUTON.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...