Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kushoto) akikagua ujenzi wa maabara ya kisasa ya Sekondari ya Mdandamo iliyopo katika Kata ya Mletele, Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma. Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Songea, Joseph Mkirikiti. Dk Nchimbi yupo mjini Songea kwa ziara ya siku tano akikagua pamoja na kufungua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopo jimboni mwake.
 Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (watatu kushoto) akiwa na Watendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea, Madiwani na viongozi wa Chama cha Mapinduzi wilayani humo wakati walipokuwa wanakagua ujenzi wa maabara, mabweni pamoja na nyumba za walimu wa Shule ya Sekondari ya Mdandamo iliyopo katika Kata ya Mletele, Manispaa ya Songea mkoani Ruvuma. Dk Nchimbi yupo mjini Songea kwa ziara ya siku tano akikagua pamoja na kufungua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopo jimboni mwake.

Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (aliyevaa mawani) akiwa na Watendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea, Madiwani na viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) wilayani humo wakilikagua daraja lililopo katika Kata ya Mletele ambalo lipo hatua ya mwisho kukamilika. Hata hivyo, Dk Nchimbi alichangia Shilingi milioni moja kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa daraja hilo. Dk Nchimbi yupo mjini Songea kwa ziara ya siku tano akikagua pamoja na kufungua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopo jimboni mwake.

 Msanii maarufu wa kuigiza sauti mbalimbali za Viongozi wa Serikali, wanasisa, watangazaji wa habari za kwenye Luninga na redio, pamoja na wasanii mbalimbali nchini, Adamu kwa jina maarufu ‘Mlugaluga’ akitoa burudani kwa wananchi wa Mtaa wa Liwumbu, Kata ya Mletele, Manispaa ya Songea kabla ya Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi (kulia) kuzungumza na wananchi hao kuhusiana na masuala mbalimbali ya maendeleo ya kata hiyo. Dk Nchimbi yupo mjini Songea kwa ziara ya siku tano akikagua pamoja na kufungua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopo jimboni mwake.
Mbunge wa Jimbo la Songea Mjini ambaye pia ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dk Emmanuel Nchimbi akizungumza na mamia ya wananchi wa Kata ya Matarawe, Mjini Songea kuhusiana na masuala mbalimbali ya maendeleo ya kata hiyo, hata hivyo Dk Nchimbi aliwahakikishia wananchi wake kuwa, kwa kushirikiana na Watendaji wa Halmashauri ya Manispaa ya Songea watalitengeza Daraja la Matarawe ambalo mara kwa mara linasababisha ajali mbalimbali zikiwemo za bodaboda.  Dk Nchimbi yupo mjini Songea kwa ziara ya siku tano akikagua pamoja na kufungua miradi mbalimbali ya maendeleo iliyopo jimboni mwake. Picha zote na Felix Mwagara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...