Rais Dkt.Jakaya Mrisho Kikwete akizungumza na mlemavu Debile James kutoka katika kijiji cha Bulega wilayani Bukombe Mkoani Geita muda mfupi baada ya kufungua shule ya msingi Ng’anzo iliyojengwa na kampuni ya madini ya Nsagali yenye makao yake wilayani humo.Rais Kikwete aliahidi kumpatia Bajaji Mlemavu huyo ili aweze kumudu shughuli zake za kujitafutia kipato. Rais Kikwete yupo katika ziara ya  siku tano mkoa mpya wa Geita kukagua na kuzindua shughuli za maendeleo.
 Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete akibonyeza kitufe kuashiria kuzindua Mkoa mpya wa Geita leo mchana.Wapili kushoto ni Naibu Waziri wa TAMISEMI anayeshughulikia elimu Kassim Majaliwa na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Geita Magalula Said Magalula.
Wazee wa Mkoa wa Geita wakimvisha Rais Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete vazi la kijadi wakati wa uzinduzi wa Mkoa Mpya wa Geita Jumamosi mchana. Picha na Freddy Maro

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Nafikiri wakati umefika kwa serikali kuwapatia bajaji walemavu wote nchini. Sio lazima mlemavu aende kwa rais kuomba.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...