![]() |
MARY JOHN MWINGIRA
5.5.1946-21.11.2010
|
”Samahani na poleni wanangu” yalikuwa ndio maneno yako kila mara na hatukuwa tunaelewa
kwa nini ulikuwa unasema vile.
Ulitufundisha kusali sala nyingi tukiwa wadogo
na tunaamini usemi wa Mapenzi ya Mungu
yametimizwa mama.
Tutaonana siku ya Mwisho Paradiso!!!
Tunaaminini upo karibu na MUNGU kama ulivyokuwa hapa duniani .Ujumbe wako mkuu uliotuachia tunajitahidi
kuuteleleza na kuishi katika hilo “Upendo usio na masharti kati yetu wanao
na wanaotuzunguka”.
Tunasema asante sana kwa malezi na maelekezo
kuhusu maisha ambayo ulikuwa unatupa kila siku ukishirikiana na baba na ndugu
na jamaa. Tunashukuru kwa Baraka za
MUNGU na tunaamini kwa maombezi
yako na baba tunamudu Maisha ya kila siku yaliyojaa Baraka tele.
Sisi wanao, wajukuu,mama yako, wakwe, Wadogo
zako, shemeji zako , ndugu na Jamaa wote tuakumbuka na Kuusifu wema wako usio na
kipimo. Tunakuadhidi kuundeleza kwa nguvu zetu zote na daima hatutakusahau Mama
yetu na Rafiki yetu Mary John Mwingira
Ustarehe kwa Amani mama yetu Mpendwa!
AMINA
Mama mwingira rest in peace
ReplyDeleteTunamshukuru Mungu kwa kila jambo, Mama ametuonesha njia ya kuishi duniani, tunaifuata. Upendo wa MUNGU uwafunike familia ya Mwingira
ReplyDeleteRIP MAMA MWINGIRA,Wote tu wasafiri, umetutangulia lakini wote tu njia moja. USTAREHE KWA Amani mama
ReplyDeleteAmen