Katibu wa Waziri Mkuu Jimbo Ndugu Charles Kanyanda akimkabidhi Sister Scholastica Mwembezi wa Masista Maria Mtakatifu Malkia wa Afika ambao ni wamiliki wa kituo cha kulea mayatima cha Katandala Mkoani Rukwa viatu pea sitini zilizotolewa na Mke wa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mama Tunu Pinda ikiwa ni ahadi aliyoitoa alipotembelea kituo hicho mapema mwaka huu. Aidha Sister Mwembezi amemuomba Katibu Kanyanda kumfikishia salamu za shukrani Mama Pinda ikiwa ni pamoja kumkumbusha ahadi ya gari aliyoitoa kwa kituo hicho.  
 Ndugu Charles Kanyanda akimvisha viatu mmoja ya watoto yatima katika kituo hicho baada ya kukabidhi zawadi hizo kutoka kwa Mama Tunu Pinda. Mzee Kanyanda amewataka wadau mbalimbali kuonyesha moyo wa upendo katika kusaidia mahitaji mbalimbali kwa watoto na kituo hicho.
Katibu wa Waziri Mkuu Jimbo Ndugu Charles Kanyanda akiimba moja ya wimbo na watoto wa kituo cha kulea mayatima cha Katandala.
(Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa @Rukwareview.blogspot.com)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...