Wakimbiza kuku ambao ni mashabiki wa Simba, Salage Mbulanzu na wa Yanga Anastella Elias wakipigwa bonge moja la chenga na Kuku wanaemkimbiza wakati wa Bonanza la ‘Nani Mtani Jembe’ lililofanyika kwenye uwanja wa Namfua wa mkoani Singida. Kuku huyo alichukuliwa na shabiki wa Simba.
Mashabiki wa Simba na Yanga wakishindana kuvuta kamba wakati wa bonanza la ‘Nani Mtani Jembe’ lililofanyika kwenye uwanja wa Namfua ulioko mkoani Singida mwishoni mwa wiki, Simba walishimba mchezo huo. Bonanza hilo lilidhaminiwa na kuandaliwa na Kilimanjaro Premium Lager.
Mashabiki wa Simba na Yanga, Igos Abdallah na Seif Omar wakishinda kukimbia na magunia kwenye mchezo huo wa kupokezana wakati wa bonanza la ‘Nani Mtani Jembe’ lililofanyika kwenye uwanja wa Namfua ulioko mkoani Singida mwishoni mwa wiki.
Mkimbiza kuku wa mashabiki wa Simba, Salage Mbulanzu akimkata kuku huku Anastella Elias akiwa hana la kufanya wakati wa bonanza la ‘Nani Mtani Jembe’ lililofanyika kwenye uwanja wa Namfua wa mkoani Singida.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...