Wakimbiza
kuku ambao ni mashabiki wa Simba, Salage Mbulanzu na wa Yanga Anastella
Elias wakipigwa bonge moja la chenga na Kuku wanaemkimbiza wakati wa
Bonanza la ‘Nani Mtani Jembe’ lililofanyika kwenye uwanja wa Namfua wa
mkoani Singida. Kuku huyo alichukuliwa na shabiki wa Simba.
Mashabiki
wa Simba na Yanga wakishindana kuvuta kamba wakati wa bonanza la ‘Nani
Mtani Jembe’ lililofanyika kwenye uwanja wa Namfua ulioko mkoani
Singida mwishoni mwa wiki, Simba walishimba mchezo huo. Bonanza hilo
lilidhaminiwa na kuandaliwa na Kilimanjaro Premium Lager.
Mashabiki
wa Simba na Yanga, Igos Abdallah na Seif Omar wakishinda kukimbia na
magunia kwenye mchezo huo wa kupokezana wakati wa bonanza la ‘Nani Mtani
Jembe’ lililofanyika kwenye uwanja wa Namfua ulioko mkoani Singida
mwishoni mwa wiki.
Mkimbiza
kuku wa mashabiki wa Simba, Salage Mbulanzu akimkata kuku huku
Anastella Elias akiwa hana la kufanya wakati wa bonanza la ‘Nani Mtani
Jembe’ lililofanyika kwenye uwanja wa Namfua wa mkoani Singida.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...