Na Dixon Busagaga wa globu ya jamii Moshi

MWANAMKE mmoja ambaye jina lake halikuweza kupatikana mara moja anayedaiwa kuwa ni mkazi wa KCMC amefariki dunia papo hapo jioni ya jana baada kugongwa na gari aina ya Fuso na kuacha njia na kisha kumgonga na kujeruhi wengine wawili.

Tukio hilo limetokea jana majira saa 12:30 jioni katika mtaa wa Posta jirani kabisa na mgahawa wa Fresh Coach huku mwili wa marehemu huyo ukishuhudiwa ukiwa chini ya gari hilo kwa takribani saa 1 kutokana na kukosekana kwa Winchi la kuinua fuso hiyo iliuweze kutolewa.

Mashuhuda waliokuwepo katika eneo la tukio hilo wamesema mwanamke huyo alikuwa ametoka katika shughuli za kibiashara katika soko lililopo mjini hapo.

Ripota wa Globu y jamii aliyokuwa maeneo ya jirani lilipotokea tukio hilo na alishuhudia gari aina ya Fuso lililosajiliwa kwa namba T 209 AHA likiendeshwa na dereva ambaye jina lake halijafahamika mara moja,likisababisha ajali hiyo iliyopelekea kifo cha Mwanamama huyo.

Chanzo cha ajali hiyo ni mwendokasi uliosababishwa na dereva wa Fuso hilo anayeonekana kabisa kuwa kalewa.

Watu wawili waliojeruhiwa kufuatia tukio hilo, ambao ni dereva wa bodaboda na rafiki yake waliokuwa wamepaki pembezoni mwa mtaa huo wakisubiri wateja.

Dereva wa Fuso hilo lililokuwa na maandishi yanayosomeka "AINULIWE BWANA" anashikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoani Kilimanjaro.

Jeshi la Polisi limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kuongeza kuwa mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya KCMC na taarifa zaidi kuhusiana na tukio hilo zitatolewa mpaka pale upelelezi utakapokamilika.
Mmoja wa Majeruhi katika ajali hiyo ambaye ni Dereva wa Bodaboda (kulia) akisaidiwa baada ya kutokea kwa ajali hiyo,huku pikipiki yake ikiwa haitamaniki.
Pikipiki nyingine nayo ni kama inavyoonekana.
Hili ndio lori lenyewe lililosababisha ajali hiyo.
Dereja wa Lori hilo (mwenye fulana nyeupe) akiwa ndani ya Gari la Polisi huku akijificha uso wake.
Mashuhuda eneo la tukio.
Namba za Usajili za Lori hilo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...