Dkt.
Sengondo Mvungi, mjumbe wa Halmashauri Kuu ya chama cha upinzani cha
NCCR-Mageuzi ambaye pia ni Mjumbe wa tume ya Katiba (pichani), amevamiwa usiku wa kuamkia leo nyumbani kwake jijini Dar es salaam na
amejeruhiwa vibaya kwa kukatwa katwa na mapanga na watu wasiofahamika ambao habari za awali zinadai kuwa ni majambazi.
Akithibitisha
tukio hilo, Mkuu wa Idara ya Itikadi na Mahusiano ya Umma wa NCCR-Mageuzi
Taifa, Mhe Moses Machali, ameiambia Globu ya Jamii muda mfupi uliopita kwamba
Dkt Mvungi alijeruhiwa vibaya sana usiku (wa kuamkia leo) saa 6.Mhe
Machali amesema taarifa zilizopatikana ni kwamba walimkata mapanga hasa
kichwani na kumsababishia kupoteza fahamu, na kwa sasa yupo Hospitali ya Taifa
ya Muhimbili kwa ajili ya matibabu.
"Wana
NCCR-Mageuzi na Watanzania wote tupeane pole kwa uvamizi wa Dkt Mvungi.
Tumwombee na kumtakia apate kupona haraka", alisema Mhe. Machali, ambaye
pia ni Mbunge wa Kasulu Mjini, akiongezea kuwa hali yake ni mbaya.



Uwii Mungu wangu mbona majanga. Jamani inasikitisha sana, Polisi tafadhali lisimamieni hili wahalifu hao wakamatwe na ku adhibishwa.
ReplyDeleteMajambazi hao waliiba kitu gani nyumbani na Dr. Mvungi? au walienda tu kwa nia la kumjeruhi? kama walienda kwa nia tu ya kumjeruhi basi hao sio majambazi wa kawaida. Tunategemea polisi watupe majibu.
Pole sana Dr, Mvungi, tunakuombea upone haraka. Poleni wana familia kwa kuuguza.
Many questions an ansewred, Get well soon ma dady
ReplyDeleteDr wa watu amewakosea nini? Jeshi la polisi naamini litatoa taarifa kamili.
ReplyDeletePole Dr wetu mungu akujalie upone haraka. Kwa nini haya yanajirudia? Inanikumbusha mwalimu wangu Dr Khidu Makubuya aliyetwambia anakaa cumpus makerere for security reasons though ana bungalow Muyenga. Watu wetu muhimu please serikali hakikisha wanakaa maeneo salama japo mmejiuzia tengeneza mengine kila mtu ajue hapa kuna serikli hata kama ni Mapinga etc. Natumaini mungu atakuponya
ReplyDeletePole sana rafiki yetu kipenzi chetu,mtetezi wetu.Mungu akupe nguvu dr.Mvungi.Wana familia pia poleni sana.amaungu atamsaidia atapona tu.Sisi rafiki zake ,tumeandaa dua ya pamoja na watoto yatima Alhamisi jioni,Ilala DSM.Mungu atamnusuru kama alivyomnusuru nabii Yunus katika tumbo la samaki, kama alivyomponyesha nabii ayub baada ya kuumwa miaka tele,na akarudi kuwa mwenye kuvutia ,INSHAA ALLAH.
ReplyDelete