Promota wa muziki jijini Koloni Bw.Peter Betram (mjerumani),amejikuta akiwekewa masharti magumu katika juhudi zake za kutaka kuandaa onyesho kubwa la muziki katikati ya jiji la Koloni,nchini Ujerumani,kwa mda wa miaka miwili sasa.

Promota huyo amekuwa akilalamikia halmashauri ya jiji kubwa la koloni kwa kumwekea ngumu katika kuandaa onyesho la muziki.

Kuanzia mwaka 2012 aliambiwa apeleke orodha ya bendi anazohitaji kuzipandisha jukwaani,baada ya kuonekana jina la bendi ya Ngoma Africa katika orodha hiyo,serikali ya jiji imemwagiza mtayarishaji wa onyesho hilo lazima akubali kuingia gharama za ziada kwa ajili ya ulinzi kutokana na msongamano wa washabiki,pia kapewa sharti lingine lazima onyesho hilo liwe nje ya mji sio kitovuni mwa jiji,kutokana na kuepuka msongamano wa washabiki wa Ngoma Africa band aka FFU ughaibuni yenye tabia za kuwadatisha akili washabiki wake.

Poromota amejikuta akivimba macho na kutojua nini? cha kufanya.

Wadaku walipo mtafuta kiongozi wa Ngoma Africa band kamanda Ras Makunja kutaka kupata mtazamo wake,kamanda alijibu kuwa kikosi chake kipo tayari tayari na wakati wowote ule watakapoitwa na poromota huyo.

Ras Makunja alikili kuwa muda wa miaka miwili Poromota amekuwa akiwapigia simu,na bendi ipo tayari kama matayarisho yatakamilika alisema Kamanda Ras Makunja, Mdodosa habari alipo hoji swala la kulikoni kamanda kumiliki bundi katika himaya ya "Anunnaki Empire" Kamanda Ras Makunja kakata simu..!!!

sijui kama aliishiwa chaji au aliondoka ki - FFU kwa mwendo wa kasi !? tu Any way tuwatafute kambini kwao www.ngoma-africa.com
Ngoma Africa band aka FFU or Anunnaki Aliens wakifanya yao jukwaani.
Kundi zima la Ngoma Africa band
Washabiki wa FFU wanatia mashaka.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Uhaiwezekani onyesho lifanyike city center katika jiji kubwa kama Koloni, kuna biashara za matajiri.
    washabiki wanaweza kuleta za kuleta

    ReplyDelete
  2. Kinacho hofiwa ni umati wa watu
    kujazana katikati ya jiji,Koloni
    wameshaona kilicho tokea kule Hamburg mwaka 2010 FFU hao hao walisababisha mtu kukanya na kufa
    baada ya watu kusongamana katika onyesho la Altona,kwa sababu lilikuwa katikati ya jiji,

    ReplyDelete
  3. FFU aka viumbe wa ajabu Anunnaki Alien bin watoto wa mbwa

    ReplyDelete
  4. vichaa wa muziki FFU ,hivi haya majina yao mbona ni ya kutisha tisha
    Anunnaki ni viumbe wa ajabu katika historia ya dunia,inasemekana walishushwa na mungu kutoka katika sayari fulani kuja ardhini kuchimba
    madini ya chuma,hawa vichaa FFU au watoto wa mbwa,pia wanaitwa Anunnaki
    Alien ! Ngoma Afrika wana vituko sana sio wanamuziki wa kikawaida

    ReplyDelete
  5. Almashauri ya koloni hawezi kuwa wendazimu waruhusu festival inafanyike kwenye shughuli za kibiashara,mbona mtayarishaji alishaelezwa lakini bado anang'angania eneo ambalo linaweza kuleta madhara

    ReplyDelete
  6. Poromota aliambiwa idadi ya askari maarumu 300 wa kutuliza ghasia wanahitajika,manspaa ya koloni haitaki kuingia gharama za juu kwa ajili ya onyesho la mtu binafsi,bendi zote ambazo zinaweza kusababisha mlindikano wa washabiki lazima zipige nje ya jiji sio katikati

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...