MAREHEMU MRS MAUA MPANKULI

Familia ya marehemu Maua Mpankuli tunapenda kutoa shukrani zetu za dhati kwa Ndugu, Jamaa, Marafiki, Wafanyakazi, Majirani na watu wote kwa ujumla waliojitoa kwa hali na mali katika msiba wa mpendwa wetu aliyeaga dunia tarehe 1 Novemba, 2013 huko Uingereza na kuzikwa katika makaburi ya Kinondoni, Dar es Salaam, Tanzania tarehe 9 Novemba, 2013.

Tunapenda kutoa shukrani zetu za kipekee kwa wafuatao:
* Madaktari na wauguzi wote wa hospitali ya St James ya Leeds, Uingereza kwa jitihada zao kubwa za kujaribu kuokoa maisha ya marehemu.

* Jumuiya ya Watanzania wote walioko Uingereza na sehemu zingine za dunia waliojitolea kwa hali na mali hadi kuweza kuusafirisha mwili wa marehemu kutoka  Uingereza hadi Tanzania kwa mazishi.
* Uongozi na waumini wa Kanisa la Christ Temple of Worship Leeds Uingereza kwa maombezi na ushikiano wao.
 * Uongozi na waumini wa Kanisa la RCCG la  Leeds, Uingereza kwa ushirikiano wao.
* Uongozi na waumini wa Kanisa la Full Gospel Bible Church, Dar es Salaam kwa huduma za kiroho wakati wote wa msiba na katika mazishi ya marehemu.
* Kampuni ya Hugh Gooding Funeral Services ya Leeds, Uingereza iliyoshughulikia kuusafirisha mwili wa marehemu kutoka Leeds hadi Dar es Salaam kwa mazishi.
* Wafanyakazi wote waliowahi kufanya kazi na marehemu katika Hospitali ya Muhimbili, Dar es Salaam.
*Jamii na viongozi wa Issamichuzi blog. Asanteni kwa kuturuhusu Kutumia mtandao wenu.
Tungependa sana kuwashukuru kila mmoja wenu kwa majina lakini kwa ajili ya wingi wenu tunaomba mpokee shukrani zetu hizi za kipekee kwa ujumla wenu.
Mwenyezi Mungu awazidishie baraka zake nyingi kwa Huduma zenu mlizotoa. Asanteni sana.
Waefeso 1: 15 – 16.

15 Hii ndio sababu nilipopata habari za imani yenu katika Bwana wetu Yesu, na juu ya upendo mlio nao kwa watu wa Mungu,16 sijaacha kumshukuru Mungu kwa ajili yenu, na kuwakumbuka katika sala zangu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...