Meneja Mauzo wa Kampuni ya Bia Tanzania (TBL) eneo la Tabata, Joseph Nicholous (kushoto) akimkabidhi mfano wa hundi yenye thamani ya sh. mil. 38, Mkurugenzi Mkuu wa Kampuni ya uchimbaji visima ya Basic Co. Ltd, Deo Bishubo kwa ajili ya gharama ya kuchimba kisima cha kina kirefu katika Zahanati ya NBC Tabata, Dar es Salaam juzi.Anayeshuhudia makabidhiano hayo ni Muuguzi Kiongozi wa Zahanati hiyo, Semeni Mtauka.PICHA ZOTE NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG
Baadhi ya wakazi wa Tabata miongoni mwao wakiwemo wagonjwa akishuhudia makabadhiano ya msaada huo
Ofisa Uhusiano wa TBL, Doris Malulu (kushoto) akielezea mikakati ya TBL ya kusaidia upatikanaji wa maji katika baadhi ya vituo vya afya na zahanati nchini.
Muuguzi kiongozi wa zahanati hiyo, Mtauka akitoa shukurani kwa TBL kuwapatia msaada wa kisima hicho kitakachosaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza tatizo la maji.
Mkazi mmoja wa Tabata akitoa shukrani kwa TBL kwa msaada huo
Zahanati ya NBC Tabata
TBL mmechemka ni Milioni Thelathini sio THELASINI
ReplyDelete