Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Mh. Dkt. Fenella Mukangara (kushoto) akipeana mkono na Balozi wa China nchini Tanzania,Mh. Lu Younqing wakati akipokea Msaada wa Pikipiki 20 zilizotolewa kwa Kampuni ya Uchapishaji wa Magazeti ya Serikali (Tanzania Standard Newspapers),wakati wa hafla fupi iliyofanyika leo nje ya Jengo la Golden Jubilee,Jijini Dar es Salaam.Kulia ni Kaimu Mhariri Mtendaji wa TSN,Gabriel Nderumaki.

Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Mh. Dkt. Fenella Mukangara (kushoto) na Balozi wa China nchini Tanzania,Mh. Lu Younqing wakiwa wamepanda pikikipi hizo ikiwa ni ishara ya kuzizindua kwa ajili ya Matumizi.Katikati yao ni Mwenyekiti wa Bodi ya TSN,Prof. Moses Warioba.
Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Mh. Dkt. Fenella Mukangara akipanda kwenye moja ya pikipiki hizo.
Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo,Mh. Dkt. Fenella Mukangara akitoa hotuba yake wakati wa hafla hiyo.
Balozi wa China nchini Tanzania,Mh. Lu Younqing akizunzumza machache wakati wa hafla hiyo.
Waziri wetu, kwa kupendeza na hizo nywele Mungu alizotujalia, endeleza mapambano!
ReplyDeleteHii misada itolewayo na hawa wenzetu akina mie.....mara nyingi mie hushindwa hata kuifurahia ..maana baada ya siku kadhaa usoni utasikia kontena limekamatwa.....sijui ndio tunabadirishana kiana...
ReplyDeleteAnony wa pili una akili finyu. Hivi watanzania walio katika magereza ya China wametumwa na Serikali ya Tanzania. By the way wengine wamekataa kurudishwa Tanzania kuja katika jela za huku wameamua kutumikia kifungo cha maisha china maana jela zao ni raha. Wacha ujinga.
ReplyDelete