Mwishoni wa wiki, Uwakilishi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa mataifa, ulitembelewa na wanafunzi wanajeshi wanane wanaoshiriki katika mafunzo ya miezi kumi, kupitia International Fellows Program yanayotolewa United States Army War war College and Carlisle Barrace. 
Chuo hicho ambacho kipo nchini Marekani, kila mwaka huanda mafunzo hayo katika ngazi ya maafisa kutoka mataifa mbalimbali marafiki. 
 Kwa mwaka huu, mafunzo hayo yanawanafunzi 367 kati yao 300 ni wamarekani na waliobaki 67 wanatoka katika mataifa mbalimbali ikiwamo Tanzania. 
Wanafunzi hao walifika katika Uwakilishi wa Kudumu wa Tanzania kama sehemu ya ziara ya mafunzo ambapo pamoja na masuala mengine, walitaka kufahamu vipaumbele vya Tanzania katika masuala muhimu yanayoikabili dunia hivi sasa ikiwani ni pamoja na matatizo yanayotokana na Mabadiliko ya Tabia nchi na matatizo ya maji kwa Afrika na namna gani Tanzania kama sehemu ya Afrika imejipanga kukabiliana nayo.
Muwakilishi wa Kudumu wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi akizungumza na sehemu ya wanafunzi wanajeshi wanaohudhuria  mafunzo ya miezi kumi katika  Chuo cha Kijeshi cha Marekani kupitia International Fellows Program, wanafunzi hao akiwamo Luteni Kanal Francis Ronald Mbindi kutoka Jeshi la  Wananchi wa Tanzania  (JWTZ) walifika  katik Uwakilishi wa Kudumu ikiwa ni sehemu ya  zaira ya mafunzo ili kujifunza  masuala mbalimbali ya kitaifa na kimataifa ambayo ni vipaumbele vya Tanzania. Kushoto kwa Balozi Manongi, ni  Naibu Muwakilishi wa Kudumu, Balozi Ramadhan Mwinyi.
Muwakilishi wa Kudumu Balozi  Manongi akisisitiza kwamba  mabadiliko  ya  Tabia nchi ( Climate Change) si suala la nadharia kwa sababu yapo matukio mengi yanayoendelea hivi sasa duniani kote ambayo ni dhahiri yanatokana na  mabadiliko hayo. akatolea mfano wa Tanzania ambako kumekuwapo na  migogoro na hata mapigano ya mara kwa mara  kati ya wakulima na wafugaji wakigombea  ardhi,   maji na malisho. Akasema migogoro kama hiyo ambayo inaathari kubwa kwa jamii za wafugaji na wakulima lakini pia hata kwa serikali kuu.  Na kwamba  inaweza kuonekana kama ni tatizo la eneo fulani au nchi fulani lakini   kama likiangaliwa katika mapana yake   dhahiri  nyuma yake ni matokeo ya   mabadiliko ya tabia nchi.  Hata hivyo akasema serikali ya Tanzania inajitahidi sana katika kujaribu kutafuta suluhu  kuhusiana na tatizo hilo ambalo anaamini linatokea pia katika nchi nyingine hususani  Afrika
Luten Kanali,  Francis Ronald Mbindi kutoka  JWTZ akitoa neno la shukrani kwa niaba ya  wenzake baada ya mazungumzo yao na  Uongozi wa  Uwakilishi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa.
4.IMG-4708. Luteni Kanal  Francis Mbindi  akimkabidhi  kwa niaba   ya wenzake, Balozi Tuvako Manongi,  sehemu ya  hotuba maarufu ya Rais Abraham Lincolin aliyoitoa  Novemba, 19, 1863 katika maadhimisho ya miaka 150 ya GettysBury  (  The turning   Point :the 150th Anniversary of the Gettysbury address) hotuba hiyo ya   Rais Lincolin inayohesabika kama hotuba muhimu sana  kuwahi kutolewa na  Rais Lincolin  ilikuwa ikielezea kuhusu vita vya wenyewe kwa  wenyewe ( CIVIL War).  vita hivyo vilivyotokea katika eneo hilo la GettysBury  vinaelezewa kama vita vilivyokuwa na umwagaji mkubwa wa damu, ambapo inasadikiwa zaidi  ya wanajeshi 50,000 waliathirika ama kwa kupoteza maisha,  kuchukuliwa mateka,  kujeruhiwa au hawakujulikana waliko
Luten Kanali,  Francis Ronald Mbindi kutoka  JWTZ akitoa neno la shukrani kwa niaba ya  wenzake baada ya mazungumzo yao na  Uongozi wa  Uwakilishi wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa.
4.IMG-4708. Luteni Kanal  Francis Mbindi  akimkabidhi  kwa niaba   ya wenzake, Balozi Tuvako Manongi,  sehemu ya  hotuba maarufu ya Rais Abraham Lincolin aliyoitoa  Novemba, 19, 1863 katika maadhimisho ya miaka 150 ya GettysBury  (  The turning   Point :the 150th Anniversary of the Gettysbury address) hotuba hiyo ya   Rais Lincolin inayohesabika kama hotuba muhimu sana  kuwahi kutolewa na  Rais Lincolin  ilikuwa ikielezea kuhusu vita vya wenyewe kwa  wenyewe ( CIVIL War).  vita hivyo vilivyotokea katika eneo hilo la GettysBury  vinaelezewa kama vita vilivyokuwa na umwagaji mkubwa wa damu, ambapo inasadikiwa zaidi  ya wanajeshi 50,000 waliathirika ama kwa kupoteza maisha,  kuchukuliwa mateka,  kujeruhiwa au hawakujulikana waliko
Wageni wetu  wakipeana   na kusaini  kitabu cha wageni, hawa wote ni wanajeshi katika ngazi ya maafisa , hawakuhitaji kukaa mezani ili kusaini kitabu
Balozi Tuvako Manongi akiendelea kubadilishana  mawazo na wageni wake,  nyuma anayeonekana kwa mbali ni Balozi  Ramadhan Mwinyi. HABARI NA PICHA NA MDAU MAURA MWINGIRA  WA UWAKILISHI WA KUDUMU WA TANZANIA  UMOJA WA MATAIFA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...