Mwenyekiti wa Kampuni ya Bravo, Abbas Mtemvu (kulia) akimkabidhi Mkazi wa Bagamoyo, Asha Vitalis tiketi ya ndege na nyaraka zingine kwa jili ya safari ya kwenda kufanya kazi Dubai, aliyotafutiwa kazi na kampuni hiyo. Hafla hiyo ya kukabidhi tiketi kwa Watanzania wawili walioondoka  kwenda kufanya kazi Dubai, ilifanyika Dar es Salaam juzi. Mpaka sasa kampuni hiyo imewatafutia kazi ughaibuni zaidi ya Watanzania 100.
 Mwenyekiti wa Kampuni ya Bravo, Abbas Mtemvu (kulia) akimkabidhi Mkazi wa Kinondoni, Neema Ndunguru tiketi ya ndege na nyaraka zingine kwa ajili ya safari ya kwenda kufanya kazi Dubai, aliyotafutiwa na kampuni hiyo. Hafla hiyo ya kukabidhi tiketi kwa Watanzania wawili akiwemo Asha Vitalis (aliyekaa kushoto) walioondoka  jana kwenda kufanya kazi Dubai, ilifanyika Dar es Salaam juzi. Mpaka sasa kampuni hiyo imewatafutia kazi ughaibuni zaidi ya Watanzania 100.
 Asha na Neema wakisikiliza kwa makini wakati Mtemvu alipokuwa akizungumza nao kuhusu ajira yao hiyo
 Mtemvu akiwa na Asha, Neema pamoja na baadhi ya wadhamini wao na baadhi ya maofisa wa Kampuni ya Bravo.
Mtemvu ambaye pia ni Mbunge wa Jimbo la Temeke, Dar es Salaam, akiwa katika picha ya pamoja na Asha (kushoto) na Neema baada ya kuwakabidhi tiketi. PICHA ZOTE NA KAMANDA WA MATUKIO BLOG.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Kweli ccmhhh wamepania kutoa ajira

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...