Muwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, Balozi Tuvako Manongi ameungana na Wawakilishi wa Mataifa mbalimbali wanaoziwakilisha nchi zao katika Umoja wa Mataifa, katika kusaini kitabu cha Maombolezo kufuatia kifo cha Rais wa Kwanza wa Afrika ya Kusini Huru, Mzee Nelson Mandela.
Kitabu hicho kimefunguliwa katika Uwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Afrika ya Kusini katika Umoja wa Mataifa. Katika Salamu zake, Balozi Tuvako Manongi ameandika " kwa niaba ya Uwakilishi wa Kudumu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika Umoja wa Mataifa, ninawasilisha salamu zetu za rambirambi kwa serikali, wananchi, familia na wapendwa wa Marehemu Mhe. Mzee Nelson Mandela.
Tunaungana nanyi katika kuombeleza msiba wa kiongozi huyo ambaye alijitolea katika kuikomboa Afrika ya Kusini. Mchango wake katika kuwaunganisha wana wa afrika ya kusini licha ya tofauti zao za kikabila ni jambo lililoihamasisha dunia yote. Sisi katika Tanzania tunajivunia sana kumfahamu Madiba".


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...