Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi la Zanzibar (SMZ), Dk. Mohamed Shein akimkabidhi tuzo Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Chiku Matesa kutokana na kutambua mchango wa shirika hilo wa kuchangia sh. milioni 100 wakati wa uzinduzi wa Mfuko wa Uwezeshaji wa Wananchi Kiuchumi Zanzibar, uliokwenda sambamba na harambee ya kuchangia mfuko huo. Hafla hiyo ilifanyika mjini Zanzibar, mwishoni mwa wiki. 
Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), Chiku Matesa (kulia), Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio (wa tatu kushoto), Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa NSSF, Juma Kintu (wa pili kushoto) wakiwa na baadhi ya wageni waalikwa katika hafla hiyo.
 Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF, William Erio (kulia), Ofisa Uhusiano Mwandamizi wa NSSF, Juma Kintu (katikati), wakiwa katika hafla ya uzinduzi wa Mfuko wa Uwezeshaji wa Wananchi Kiuchumi Zanzibar, iliyokwenda sambamba na harambee ya kuchangia mfuko huo. 
Rais Dk, Shein akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Mashirika na Taasisi mbalimbali zilizochangia Mfuko wa Uwezeshaji Zanzibar.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...