Niseme wazi kwamba timu yetu iko kwenye maandilizi ya mwishomwisho kabisa kabla ya kuumana na watani wetu wa jadi, Wahenga Veterans, hii itakuwa na game number 566U itakayopigwa uwanja wa TP Tandale alimaarufu Nangwanda sijaona.
Itakumbukwa kwamba mwaka jana mechi kama hii wenzetu walishinda kwa goli za jioni sana, kwakutambua hilo walimu wetu akina Madaraka Selemani wamefanya kazi ya ziada kwa kurekebisha baadhi makosa na vilevile kucheza mechi nyingi sana za kirafiki ikiwa ni pamoja na kuvuka maji hadi visiwani tulipowapiga KMKM 2-1.
Tarehe
|
Muda
|
Mechi No
|
Uwanja
|
mechi Na
|
21/12/2013
|
0800am
|
564U
|
Staki Shali
|
Staki shali Veterans
|
22/12/2013
|
0430pm
|
565H
|
Nagwanda Sijaona a k a TP
|
Kilwa Veterans
|
28/12/2013
|
0430pm
|
566U
|
Nagwanda Sijaona a k a TP
|
Wahenga Veterans
|
Timu iko sawasawa kutoa burudani kwa wapenzi wetu karibuni sana.
Pamoja na maandilizi hayo tunapenda kuwafahamisha kwamba Golden Bush tumemchukua bwana Jonas Afumwisye kuwa bounsa wetu hasa pale tunapocheza game nzito hasa zenye upinzani kama Wahenga.
Asanteni
Onesmo
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...