MASHINDANO ya Michezo kwa Vyuo vya Elimu ya Juu Tanzania (SHIMIVUTA), yanatarajiwa kupihwa mkoani Tanga kuanzia Desemba 6 hadi 21 mwaka huu.

Mashindano hayo hujumuisha michezo ya soka, netiboli, mpira wa kikapu, mpira wa wavu, huku riadha na pooltable vikitarajiwa kuongezwa kwa mara ya kwanza msimu huu.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Rais wa Shimivuta, Mwalimu Rashid, alisema vyo 25 vimetumiwa mialiko kwa ajili ya kushiriki katika mashindano hayo. Mwalimu alisema tayari vyuo hivyo vimeanza kutbibitisha ushiriki wao, ambapo ratiba ya michezo yote itapangwa siku moja kabla ya kuanza kwa michuano hiyo.

"Tumepanga kupanga ratiba hivyo kuepuka usumbufu wa siku ya mwisho, timu nyingi zimethibitisha kushiriki na tumeongeza michezo miwili tuone kama itawezekana.

"Lakini licha ya kuitaja michezo hii tuklioiongeza, Kamati ya Utendaji inakutana Desemba 4 kwa ajili ya kuangalia jinsi ya kuiweka michezo hii ya pooltable na riadha kwa mafanikio," alisema Mwalimu.

Rais huyo aliongeza kuwa changamoto kubwa wanayokutana nayo kwa sasa ni kutojitokeza kwa wadhamini licha ya kuwaomba mara kwa mara kuwaangalia katika uendeshaji wa michezo hiyo ya vyuo vya elimu ya juu.

Mwalimu alimtaja mgeni rsmi katika uzinduzi wa michezo hiyo katika Uwanja wa CCM Mkwakwani kuwa atakuwa Mkuu wa Wilaya ya Tanga.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...