Washiriki wa Warsha ya siku mbili ya kujenga uelewa wa mpango wa kunusuru Kaya Maskini kwa wahariri na waandishi wa habari wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa TASAF Ladislaus Mwamanga (wa tatu toka kushoto waliyokaa).
  Mkurugenzi Mtendaji wa TASAF Bw. Ladislaus Mwamanga akifungua Warsha ya siku mbili ya kujenga uelewa wa mpango wa kunusuru Kaya Maskini kwa wahariri na waandishi wa habari (hawapo pichani) inayofanyika katika Hoteli ya Oceanic Bay & Resort mjini Bagamoyo.
Mwenyekiti wa siku ya kwanza ya warsha ya kujenga uelewa wa mpango wa kunusuru Kaya Maskini kwa wahariri na waandishi wa habari ambaye ni Mhariri wa Channel Ten Ester Zelamula (katikati aliyeshika mic) akifafanua jambo kwa washirki (hawapo pichani), wa kwanza kushoto kwake ni Mkurugenzi Mkuu wa TASAF Ladislaus Mwamanga na wengine ni wakurugenzi wa idara mbalimbali wa TASAF.
 Kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa uratibu Bw. Alphonce Kyariga, Mkurugenzi wa Ukaguzi Christopher Sanga na Kaimu Mkurugenzi wa Kujenga Uwezo Fariji Mishael wakifuatilia kwa makini uwasilishwaji wa mada katika warsha ya kuwajengea ufahamu wanahabari.
 Baadhi ya washiriki wa Warsha ya siku mbili ya kujenga uelewa wa mpango wa kunusuru Kaya Maskini kwa wahariri na waandishi wa habari wakifuatilia uwasilishwaji wa mada mbali mbali katika hoteli ya Oceanic Bay & Resort Mjini Bagamoyo.PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...