Mkurugenzi Mkazi wa USAID,
Sharon L. Cromer ameahidi kuendelea kushirikiana na TFDA katika kuhakikisha
afya ya wananchi inalindwa kwa kuisaidia Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA) katika
kuijengea uwezo kwenye masuala ya udhibiti wa usalama na ubora wa bidhaa za
chakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba nchini.
Kauli hiyo imetolewa leo tarehe
17/12/2013 katika ziara ya ujumbe wa USAID iliyofanyika Makao Makuu ya TFDA kwa
lengo la kujionea ufanisi wa utendaji wa Mamlaka kufuatia misaada mbalimbali
ambayo imekuwa ikitolewa na Shirika hilo la kimaendeleo kwa TFDA kuanzia mwaka
2011 hadi sasa.
USAID imekuwa ikiisaidia TFDA
katika kuwajengea uwezo watumishi wake hususan udhamini wa mafunzo kwa wakaguzi
wa dawa, mafunzo kwa watumishi kuhusu mifumo bora ya utendaji kazi na utoaji
huduma pamoja na manunuzi ya vifaa vya maabara ya Mikrobiolojia kwa lengo la kuendelea
kukidhi vigezo vya Shirika la Afya Duniani (WHO).
Naye Mkurugenzi Mkuu wa TFDA,
Hiiti B. Sillo, alikabidhi tuzo maalum kwa shirika la USAID ikiwa ni alama ya
kutambua mchango wa USAID katika mafanikio yaliyofikiwa na Mamlaka kwa kipindi
cha miaka 10 (2003-2013).
Mkurugenzi
Mkuu wa TFDA, Hiiti B. Sillo akikabidhi tozo maalum kwa Mkurugenzi wa USAID Bi.
Sharon L. Cromer katika hafla iliyofanyika TFDA makao Makuu.
Sehemu
ya wajumbe wa Menejimenti ya TFDA na ujumbe wa USAID wakiwa katika picha ya
pamoja mara baada ya ziara hiyo.
Mkurugenzi
Mkuu wa TFDA, Hiiti B. Sillo akiuonesha ujumbe wa USAID moja ya vitabu rejea
vya viwango vinavyotumika katika maabara ya TFDA.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...