Mwakilishi kutoks IOGT-NTO, Gunnar Lundstom akiwasilisha mada katika kongamano juu ya kudhibiti matumizi
mabaya ya pombe kwa mkoa wa Iringa lililoandaliwa na shirika lisilo la
kiserikali la Iringa Development of Youth Disabled and Childen Care (IDYDC) na
kufanyika katika ukumbi wa Valentine mjini Iringa.
Mganga wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa
Iringa na Mratibu wa madhara ya pombe afya mkoa,Dk. Ally Ngala akizungumza katika kongamano juu ya kudhibiti matumizi
mabaya ya pombe kwa mkoa wa Iringa lililoandaliwa na shirika lisilo la
kiserikali la Iringa Development of Youth Disabled and Childen Care (IDYDC) na
kufanyika katika ukumbi wa Valentine mjini Iringa.
Baadhi ya wajumbe waliohudhuria kongamano juu ya kudhibiti matumizi
mabaya ya pombe kwa mkoa wa Iringa lililoandaliwa na shirika lisilo la
kiserikali la Iringa Development of Youth Disabled and Childen Care (IDYDC) na
kufanyika katika ukumbi wa Valentine mjini Iringa.
======== ====== ========
WATU MILIONI 2 HUFARIKI DUNIA KWA POMBE
Na Denis Mlowe na Pauline Kuye, Iringa
UTAFITI uliofanywa na serikali kupitia Wizara ya Afya imebainika
kuwa watu milioni mbili hufariki
kila mwaka duniani kutokana na matumizi ya pombe.
Hayo yameelezwa na Mganga wa Hospitali ya Rufaa ya
Mkoa wa
Iringa Dk. Ally Ngala wakati akizungumza katika kongamano juu ya kudhibiti matumizi
mabaya ya pombe kwa mkoa wa Iringa lililoandaliwa na shirika lisilo la
kiserikali la Iringa Development of Youth Disabled and Childen Care (IDYDC) na
kufanyika katika ukumbi wa Valentine mjini hapa.
Dk.Ngala alisema asilimia 4 ya magonjwa yasiyo ya kuambukizwa husababishwa na matumizi mabaya ya
pombe kupita kiasi na kusababisha madhara mengi zaidi kwa watumiaji wa
pombe ikiwemo mama wajawazito kuzaa mtoto kabla ya miezi tisa (njiti).
Alisema utafiti
huo ulifanywa Februari
na Octoba 2012 ulibainisha asilimia 26.8 mpaka 31.9 sawa na
watu milioni 15 nchini Tanzania wanatumia pombe, na kati ya hao asilimia 27.4 ya
wanaume wanywaji wa pombe ni walevi kupindukia na huku wanawake ikiwa ni asilimia 13.4.
Aidha Ngala alisema hunywaji wa pombe una hasara nyingi na kubwa sana kuliko faida zake na alibainisha
kuwa hasara mbaya za pombe kwa
mtumiaji ni upande wa kiafya.
“Pombe ina hasara kubwa sana kwa binadamu kiuchumi kwa
kusababisha umaskini kifamilia lakini kwa upande wa afya ndio zaidi hii inatokana na kuwa na mchango mkubwa
katika kuleta magonjwa, ingawa sio kila ugonjwa husababishwa na pombe
pekee” alisema Dk. Ngala
Ngala alisema madhara mengine ya unywaji wa pombe kupita
kiasi ni kusababisha ugonjwa wa Ini kwa kufa kwa seli za ini hivyo baadaye ini
linapoteza uwezo kabisa kwa kushindwa kufanya kazi hivyo kusababisha
vifo vingi kwa ugonjwa huo.
Alibainisha pombe husababisha kansa za tumbo na kansa ya
kongosho na mtumiaji wa pombe kwa kiasi kikubwa watoto huzaliwa katika hali ya utegemezi wa pombe(Fotal alcoholic syndrome)
ambayo huweza kumpotezea maisha mtoto ndani ya mwezi wa kwanza au utaahira wa kudumu(matatizo ya akili).
Alisema pombe huathiri kiasi kikubwa watumiaji mfumo mzima wa uzazi na hata kupelekea
mtumiaji kupoteza uwezo wa kuzaa kabisa, na huanzia kupoteza siku za hedhi kwa mwanamke.
Aliongeza madhara mengine ya unywaji wa pombe kupita kiasi
ni chanzo kikubwa cha ajali za barabarani na kusababisha hasara kubwa kwa taifa
kwa ujumla.
What? fotal????, it should have been foetal
ReplyDelete