Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akiwahutubia wanafunzi wa Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Chukwani nje kidogo ya Mji wa Zanzibar waliomaliza masomo yao ya shahada ya kwanza kwenye mahafali ya 13 ya chuo hicho.Kushoto ya Balozi Seif ni Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Mh. Ali Juma Sahamuhuna na kulia yake ni Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho Dr. Abdulrahman El- Muhailan.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif akikabidhi zawadi kwa baadhi ya wanafunzi bora wa masomo mbali mbali waliofanya vizuri kwenye masomo yao ya shahada ya kwanza katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Elimu Chukwani. Kulia yake wanaofurahia ni Mwenyekiti wa Baraza la Chuo hicho Dr. Abdulrahman El – Muhailan na Mkuu wa Chuo Kikuu chukwani Profesa Hamed Rashid Hikman.
Baadhi ya wanafunzi wa chuo Kikuu Shirikishi cha Elimu chukwani wakiwa katika madaha kwenye mahfali yao ya 13 ya kumalizia masomo yao ya shahada ya kwanza.
Wanafunzi wa Chuo Kikuu shirikishi cha elimu chukwani wa fani ya Geagraph wakiwa katika vitendo vya kuashiria kukamilisha masomo yao ya shahada ya kwanza chuoni hapo. Picha na Hassan Issa wa – OMPR – ZNZ.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Chuo kikuu cha elimu kilioni?? Duh!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...