Bendi ya Mlimani Park Orchestra almaarufu kama Sikinde inategemea kuburudisha wapenzi wa muziki wa dansi kutoka Dar es Salaam kesho Ijumaa (31 Januari 2014) katika ukumbi wa Meeda Sinza wilayani Kinondoni.

Akizungumza kwa niaba ya bendi ya Sikinde, Katibu wa bendi hiyo Hamis Mirambo amesema “baada ya kukaa muda mrefu bila kufanya shoo yeyote katika wilaya ya Kinondoni ,bendi ya Sikinde sasa ipo tayari kuwakosha moyo za wapenzi wa muziki wa dansi katika wilaya hiyo pamoja na watu wa wilaya za jirani.”

“Tunapenda kuwaalika wapenzi wote wa muziki wa dansi wasikose kuhudhuria shoo yetu ambayo itaanza ukumbini Meeda kuanzia saa mbili usiku,” alisema Mirambo.

Aliongeza, “Karibuni mpate kuburudika na nyimbo za zamani na mpya kutoka bendi hii kongwe hapa nchini. Mpate kusikia kutoka kwa msanii Bichuka na wengine wengi…karibuni sana!”

Kwa hivi sasa bendi hiyo ya Mlimani Park Orchestra inamalizia kukamilisha albamu yao mpya iitawayo “Jinamizi la talaka” ambayo inabeba nyimbo kama Kibogoyo, Deni ntalipa, Ng’ombe haelemewi nunduwe, Kukatika kwa dole gumba, Tabasamu na Mkwezi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Safi sana, Tunafurahi sana sana Wazee wa Nginde , Karibuni sana Meeda mje mtupe Burudani, ila wengine kama sisi hata mkipiga wapi tupo pamoja
    Dr Ntamamiro Zephania Mzee wa Nginde

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...