Mkurugenzi Mkuu wa COSTECH Dr Hassan Mshinda akifafanua mbele ya wajumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundo mbinu waliotembelea COSTECH mapema leo jinsi COSTECH inavyojitahidi kusomesha watafiti ili kukabiliana na tatizo la uhaba wa Watafiti nchini .Kwa kipindi cha mwaka  2010 hadi 2013  COSTECH imesomesha jumla ya Watafiti 386 kutoka Taasisi za Utafiti na Vyuo Vikuu kwa shahada ya Uzamili na uzamivu.Mwaka 2013/2014 Jumla ya Watafiti 131 wamekwishafadhiliwa na COSTECH wakiwemo 85 wa shahada ya uzamili na 46 wa shahada ya uzamivu.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Mawasiliano Sayansi na Teknolojia Dr Patrick Makungu akitoa ufafanuzi kwa Kamati ya Bunge juu ya namna COSTECH iliyo chini ya wizara yake  inavyokutana na changamoto ya kushuka kwa fedha za kugharamia utafiti kila mwaka.

 Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundo mbinu Mh Zarina Shamte Madabida akipata ufafanuzi juu ya kazi zinazofanywa na Atamizi ya Dtbi iliyopo chini ya COSTECH.
Mkurugenzi wa Ubunifu,Ujasiriamali na Ushindani wa COSTECH Dr Dugushilu Mafunda(katikati) akitoa ufafanuzi kwa Mjumbe wa Kamati ya Bunge ya Miundo Mbinu Mh Rebecca Michael Mgodo(wa kwanza kulia)  jinsi Kurugenzi yake inavyofanya kazi za kuendeleza ubunifu,ujasiriamali na Ushindani nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...