Muanzilishi wa Flaviana Matata Foundation (FMF),ambaye ni Mwanamitindo wa Kimataifa,Flaviana Matata akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) katika mkutano uliofanyika kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Serena Jijini Dar es Salaam leo,wakati akizungumzia mradi wake unaotambulika kama “FMF Stationeries Project”; mradi unaojihusisha na uhamasishaji wa mashirika mbalimbali, taasisi za serikali na watu binafsi kuchangia na kusambaza vifaa mbali mbali vya shule kama vile madaftari ya mazoezi, kalamu za wino, kalamu za risasi, rula, mikebe, vifutio na mabegi ya wanafunzi, kwa wanafunzi wanaosoma katika mazingira magumu hapa nchini Tanzania.
Afisa Mawasiliano,Masoko na Uenezi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF,Hawa Kikeke (kushoto) akizungumza na akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na jinsi Mfuko huo ulivyoweza kushirikiana na Flaviana Matata Foundation katika kusaidia kuinua elimu hapa nchini,ambapo kwa ushirikiano huo wamefanikiwa kusambaza vifaa vya shule (stationery kits) vinavyojumuisha mabegi ya shule, madaftari ya mazoezi na vitu vingine,Katika awamu ya kwanza ya mradi (Januari 2014) PSPF wamechangia “FMF Stationery kits” 1000 kwa wanafunzi wasiojiweza mkoani Pwani.
Mratibu wa Flaviana Matata Foundation (FMF),Lusajo Mwaisaka akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusiana na Mpango Mkakati wa Flaviana Matata Foundation kuendelea kusaidia wanafunzi wasiojiweza katika maeneo mbali mbali hapa nchini.Kushoto ni  Muanzilishi wa Flaviana Matata Foundation (FMF),ambaye ni Mwanamitindo wa Kimataifa,Flaviana Matata.
 Muanzilishi wa Flaviana Matata Foundation (FMF),ambaye ni Mwanamitindo wa Kimataifa,Flaviana Matata pamoja na Afisa Mawasiliano,Masoko na Uenezi wa Mfuko wa Pensheni wa PSPF,Hawa Kikeke  wakifurahia jambo wakati wa kupata picha ya pamoja.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Safi sana mdogo wangu Flaviana. Natumai nasi tukishirikiana na mashirika mengine tutaweza kuiga mfano wako.

    Che

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...