Juma Makongoro ambaye Mkuu wa Doria za Uvuvi Kanda ya Mwanza akimkumbatia mama mmoja kati ya wazee wa Kituo cha kulelea wazee cha Kalwande kilichopo Usagara Bukumbi wilayani Misungwi mkoani Mwanza ambapo yeye pamoja na rafiki zake wakiwemo wengine toka sekta ya uvuvi pamoja na wafanyabiashara walitembelea kituo hicho kwaajili ya kula pamoja na kutoa misaada kama sehemu ya kusherehekea mwaka mpya 2014.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Misungwi Bernard Polycap akizungumza na wazee wa Kituo cha kulelea wazee cha Kalwande kilichopo Usagara Bukumbi wilayani Misungwi mkoani Mwanza ambapo yeye aliwaasa wazee hao kuunda vikundi  kwa kuzingatia vipaji vyao na kujiorodhesha ili ofisi yake itizame jinsi ya kuwawezesha mitaji midogo midogo itakayo wasaidia kuanzisha miradi ya kujikimu kwa mahitaji binafsi.

Juma Makongoro ambaye Mkuu wa Doria za Uvuvi Kanda ya Mwanza (kulia) akimkabidhi msaada wa nguo Bi.Angelina Jonas katika sherehe ya kuukaribisha mwaka mpya 2014 iliyofanyika katika Kituo cha kulelea wazee cha Kalwande kilichopo Usagara Bukumbi wilayani Misungwi mkoani Mwanza. Kushoto ni Mkurugrnzi wa kituo hicho. 
Makabidhiano yakiendelea katika kituo cha kulelea wazee cha Kalwande kilichopo Usagara Bukumbi wilayani Misungwi mkoani Mwanza, ambapo zawadi za nguo, mafuta, sabuni, mchele, unga na bidhaa nyinenezo gawiwa kwa mabalozi wa wazee hao ambapo kila balozi anakaa na watu wake kisha wana gawana kwa usawa.
Picha ya pamoja ya kamati ya wadau walio fanikisha sherehe hiyo.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...