Wawakilishi wa Kudumu kutoka nchi 193 wanaoziwakilisha nchi zao katika Umoja wa Mataifa, wakimsikiliza Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki Moon wakati alipolizungumza Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa siku ya Ijumaa. Alitumia fursa hiyo, kuainisha vipaumbele vyake vya mwaka 2014, mafanikio na changamoto zinazoukabili Umoja wa Mataifa ikiwamo migogoro inayoendelea huko Sudan ya Kusini, Jamhuri ya Afrika ya Kati na kwingineko Duniani. Akatahadharisha kwamba kama Jumuiya ya Kimataifa haitakuwa makini kuna hatari kubwa ya kutokea mauaji makubwa ya raia kama ambavyo imeshawahi kutokea huko nyuma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. 'CoW' Kazi kwenu Msala ndio huo unaendelea kuchanika!

    Sudani yaKusini hali tete, si ndio ninyi Kenya ,Uganda na Rwanda mlikuwa mnalazimisha bila kutimiza Vigezo Sudani Kusini ipewe Uanachama EAC?

    ReplyDelete
  2. Kuacha ukabila, udini na ubabe wa kisiasa ni somo linalotokana na matukio ya Southern Sudan na Central African Republic.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...