Mkuu wa Mkoa wa Rukwa Injinia Stella Manyanya akizungumza kwenye kikao na watumishi wa idara ya afya wa hospitali kuu ya Mkoa iliyopo katika Manispaa ya Sumbawanga. Alisema kuwa lengo la kikao hicho ni kusikiliza kero, malalamiko pamoja na ushauri kwa ajili ya kuboresha huduma na utendaji katika hospitali hiyo. Kero mbalimbali zilitolewa ikiwepo upandishwaji wa vyeo kuchukua mda mrefu, kubadilishiwa muundo wa vyeo na kusababisha kupungua kwa mishara kimakosa, uhaba wa vitendea kazi pamoja na madaktari bingwa wa upasuaji ambapo kwa sasa hamna hata mmoja.
Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Rukwa Ndugu Samson Mashalla akifafanua baadhi ya mambo ya kiutawala katika kikao hicho.
Wajumbe katika kikao hicho.
Mmoja ya wahudumu wa afya akitoa kero yake.(Na Hamza Temba - Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Rukwa)
Ankal mithupu una ubia na huyu mama?
ReplyDeleteafisa alievaa suti ya kijivu kwenye picha ya kwanza, inaelekea yuko kwenye face book wakata mkuu wake akitoa hotuba. chunga!
ReplyDelete