Meneja wa Fedha wa Benki ya NMB, Deogratias Usangira akipokea Tuzo kutoka kwa Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe.Goodluck Ole Medeye. Benki ya NMB imepokea tuzo hii ya ushindi wa kwanza wa kuwasilisha taarifa ya fedha ya mwaka 2012 kutoka kwenye Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi wa Mahesabu nchini. Hafla hii ya makabidhiano ilifanyika hivi karibuni mkoani Arusha.
Maafisa wa benki ya NMB (toka kushoto) Evarist Webby, Jonathan Eliamlisi, Deogratias Usangira na Israel Kingu wakiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kupokea tuzo hii ya ushindi wa kwanza wa kuwasilisha taarifa ya fedha ya mwaka 2012 kutoka kwenye Bodi ya Wahasibu na Wakaguzi wa Mahesabu nchini katika hafla ya makabidhiano iliyofanyika hivi karibuni mkoani Arusha.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...