Na Benjamin Sawe,WHVUM
“Vijana ni nguvu kazi ya Taifa”. Hii ni kweli na kwa mujibu wa utafiti wa Nguvu Kazi Nchini ya mwaka 2006 asilimia 68% ya nguvu kazi nchini ni Vijana ambao idadi yao kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 ni 15,587,621 sawa na asilimia 34.7% ya idadi ya watu wote nchini. Kati yao Vijana wa kike ni 8,273,505 sawa na asilimia 35.9% na Vijana wa kiume ni 7,314,116 sawa na asilimia 33.4%.
Kutokana na umuhimu huu, kumekuwa na jitihada mbalimbali za Serikali zinazolenga katika masuala ya maendeleo ya Vijana nchini hii ikiwa ni pamoja na kuwa na Sera, Mipango na Mikakati inayokidhi mahitaji mbalimbali ya vijana kama vile, Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana 2007,Sera ya Taifa ya Ajira 2008 (Iliyo chini ya Wizara ya Kazi na Ajira), Mpango Kazi wa Taifa wa Ajira kwa Vijana 2007 na Programu ya Kukuza Ajira zenye Staha kwa Vijana nchini inayoratibiwa kati ya Wizara Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na Shirika la Kazi Duniani (ILO).
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana Bw. James Kajugusi anasema Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana 2007 ni matokeo ya maboresho ya Sera ya Vijana ya mwaka 1996 ambapo, maboresho ya Sera hiyo yanatokana na mabadiliko, mahitaji au changamoto mbalimbali zinazojitokeza za kijamii, kiuchumi na kisiasa.
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
“Vijana ni nguvu kazi ya Taifa”. Hii ni kweli na kwa mujibu wa utafiti wa Nguvu Kazi Nchini ya mwaka 2006 asilimia 68% ya nguvu kazi nchini ni Vijana ambao idadi yao kwa mujibu wa Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 ni 15,587,621 sawa na asilimia 34.7% ya idadi ya watu wote nchini. Kati yao Vijana wa kike ni 8,273,505 sawa na asilimia 35.9% na Vijana wa kiume ni 7,314,116 sawa na asilimia 33.4%.
Kutokana na umuhimu huu, kumekuwa na jitihada mbalimbali za Serikali zinazolenga katika masuala ya maendeleo ya Vijana nchini hii ikiwa ni pamoja na kuwa na Sera, Mipango na Mikakati inayokidhi mahitaji mbalimbali ya vijana kama vile, Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana 2007,Sera ya Taifa ya Ajira 2008 (Iliyo chini ya Wizara ya Kazi na Ajira), Mpango Kazi wa Taifa wa Ajira kwa Vijana 2007 na Programu ya Kukuza Ajira zenye Staha kwa Vijana nchini inayoratibiwa kati ya Wizara Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo na Shirika la Kazi Duniani (ILO).
Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Vijana Bw. James Kajugusi anasema Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Vijana 2007 ni matokeo ya maboresho ya Sera ya Vijana ya mwaka 1996 ambapo, maboresho ya Sera hiyo yanatokana na mabadiliko, mahitaji au changamoto mbalimbali zinazojitokeza za kijamii, kiuchumi na kisiasa.
BOFYA HAPA KUSOMA ZAIDI
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...