Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk. Pindi Chana akimsikiliza kwa makini Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya, Hamis Mdee muda mfupi baada ya kutembelea banda la Mfuko huo.
Ofisa Matekelezo Desiderius Buhiye akitoa maelezo ya shughuli zinazofanywa katika banda la NHIF kwa Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk Pindi Chana.
Baadhi ya washiriki wa maadhimisho ya miaka 50 ya Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru wakiendelea kupata huduma ya kupima afya zao.
Upimaji ukiendelea
Ofisa Matekelezo wa NHIF akitoa elimu kwa Maofisa wa Maendeleo ya Jamii waliofika bandani hapo kupata ufafanuzi wa mambo mbalimbali.

SERIKALI imesema itaendelea kuunga mkono juhudi zinazofanywa na Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) hususan za kuhamasisha wananchi kujiunga na Mfuko huo pamoja na Mfuko wa Afya wa Jamii (CHF) ili wanufaike na huduma za matibabu.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk. Pindi Chana wakati alipotembelea banda la NHIF katika Maadhimisho ya Miaka 50 ya Chuo cha Maendeleo ya Jamii Tengeru ambayo yamekwenda sambamba na Mkutano Mkuu wa Maofisa Maendeleo ya Jamii nchini.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...