Marehemu Jane Lillian Samatta
Familia ya Mh. Jaji Mkuu Mstaafu Barnabas A. Samatta inatoa shukrani zetu za dhati kwa wale wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine, katika kuwafariji katika msiba wa mpendwa wao, Jane Lilian Samatta, aliyefariki tarehe 09 Disemba, 2013, katika Hospitali ya TMJ hapa Dar Es Salaam.

Shukrani za kipekee ziwafike wafuatao: Mh. Jaji Mkuu wa Tanzania Mohamed Chande Othman; Mh. Jaji  Mkuu wa Zanzibar Omar Othman Makungu; Waheshimiwa Majaji wa Mahakama kuu ya rufaa na wa Mahakama kuu; Waheshimiwa Majaji Wastaafu; Mtawala Mkuu wa Mahakama Bw. Hussen Kattanga; Waziri wa mambo ya nje na ushirikiano wa kimataifa Mh. Bernard Membe; Prof. Mkude, Mwenyekiti wa Baraza la Chuo Kikuu Mzumbe; Prof. Joseph Kuzilwa, Makamu Mkuu wa Chuo na Makamu wake, Prof. F. Kamuzora na Prof. J.S. Itika, na jumuia ya chuo Kikuu hicho cha Mzumbe.
Mh. Makamu Mwenyekiti wa Judges and Magistrates Vetting Board ya Kenya
Bi. Roseline Odede, Mh. Mjumbe na Mtendaji Mkuu wa Bodi hiyo, Waheshimiwa Justus Munyithya na Reuben Chirchir, pamoja na Viongozi wengine na Watumishi wa Bodi hiyo;
 Meneja Mkuu wa Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC) Bw. Abdo Majd, Viongozi na Watumishi wote; Menejimenti na Watumishi wa Management And Development For Hearth (MDH);
Walimu na Watumishi wa Shule ya Msingi ya Libermann; Madaktari na Wauguzi wa Hospitali ya TMJ; Dr. Mwandolela, Dr. Paschal na Wauguzi wa Heameda Medical Clinic; Majirani wa Mtaa wa Bongoyo na Mitaa ya jirani; Majirani wa Oyster Bay Neighborhood Association (CONA); Vikundi vya  Green Women na Great Sisters; Wanajumuia wa Jumuia ya Mtakatifu Agostino wa Hippo; Bi. Eliaebeth Mwella; Bw. Aaron Tesha; Bi. Diana Mkapa; Bi. Magdalena Ingi; Bi. Gloria Sindano; Viongozi, Kwaya ya Kanisa na Waumini Kanisa Kuu la Mtakatifu Albano; Ndugu, Jamaa na Marafiki.
IBADA YA SHUKRANI
 Itafanyika katika kanisa kuu la mtakatifu Albano jijini Dar es salaam kesho Jumamosi saa 2 asubuhi  tarehe 11 January 2014. 
MPENDWA WETU JANE, MIKONONI
MWA MWENYEZI MUNGU PUMZIKA,

MIOYONI MWETU ISHI DAIMA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 7 mpaka sasa

  1. RIP Dada Jane, Missing u so much!

    ReplyDelete
  2. R.I.P Jane!

    ReplyDelete
  3. Soo beautiful yet gone, Rest in Peace Jane.

    ReplyDelete
  4. Our collective hearts are heavy with over Jane's death. She was such a great person,gone too soon. Lets her live on in our memories forever.

    ReplyDelete
  5. Rest In Peace Jane...

    Poleni sana Familia ya Rt Jugde Samatta - she has gone too soon... Tulikuwa pamoja enzi Za kusoma Tabora!

    Mwenyenzi Mungu mwingi wa rehema awape faraja na ustahmilivu katka kipindi hiki kigumu sana kwenu!

    Bwana alitoa na bwana ametwaa - Jina lake lihimidiwe.

    ReplyDelete
  6. Aisee naona familia ya Mheshimiwa imekuwa kwenye kipindi kigumu ukizingatia muda si mrefu ulopita mliondokewa na kijana wenu mpendwa.

    Mungu awape nguvu kipindi hiki kigumu...Dunia ni mapito

    RIP

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...